Ruka hadi kwenye maudhui makuu

LIVERPOOL KUWANUNUA ORIGI NA MARKOVIC, SUAREZ ANAKWENDA BARCELONA

Liverpool ya Uingereza imekubaliana na klabu ya Lille kumsajili mshambulizi wa Ubeljiji ambaye ni mzaliwa wa Kenya Divock Origi .


Timu hiyo vilevile inapania kumsajili kiungo cha kati wa Serbia na Benfica Lazar Markovic .
The Reds wamekubalia kutoa kitita cha pauni milioni £10m kwa tineja huyo 19 Origi.
Origi hata hivyo anatarajiwa kukamilisha mazungumzo juma lijalo .
Klabu hiyo vilevile inapania kukamilisha makubaliano na Markovic, ambaye ataigharimu takriban pauni milioni £25m.
Mazungumzo ya wawili hao yanawadia huku ikifahamika kuwa Liverpool inatarajia kumuuza mfungaji mabao mengi katika msimu uliopita katika ligi ya Uingereza Luis Suarez, kwa Barcelona kwa pauni milioni £75m.
Barca imeonesha niya ya kumnunua Suarez fauka ya matatizo yaliyokumba baada ya kumngata mlinzi wa Italia Chiellini katika mechi ya kombe la dunia .

Liverpool vilevile inamtaka Alexis Sanchez, katika uhamisho huo wa Suarez .
Suarez anahamia Barcelona
Liverpool tayari imewanunua Rickie Lambert,32, kiungo Adam Lallana ,kutoka Southampton kwa gharama ya pauni ya milioni £29m.

Emre Can,20, vilevile ameshadunda Anfield.
Kocha Brendan Rodgers anatafuta kuimarisha kikosi chake kabla ya kushiriki mchuano wa kuwania ubingwa wa bara uropa mwakani baada ya kumaliza katika nafasi ya pili msimu uliopitanyuma ya Manchester City.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...