Ruka hadi kwenye maudhui makuu

IVO MAPUNDA AMUHOFIA CASSILAS


Kipa chaguo la kwanza wa timu ya Simba ya jijini Dar es Salaam, Ivo Mapunda, amesema kwamba anamhofia kipa mpya aliyetua kwenye kikosi hicho, Hussein Shariff 'Casillas' kutoka Mtibwa Sugar ya Manungu mkoani Morogoro.

Casillas alisaini mkataba mpya wa miaka miwili wa kuitumikia Simba mwishoni mwa wiki iliyopita.

Akizungumza na gazeti hili, Mapunda, alisema kwamba Casillas ndiye kipa bora wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu uliopita hivyo atajipanga kufanya mazoezi ili kulinda kiwango chake na kujihakikishia namba katika kikosi cha kwanza.


Mapunda ambaye aliwahi kuzichezea timu za Prisons ya Mbeya, Yanga ya jijini na St. George ya Ethiopia alisema kuwa hatabweteka na atahakikisha anapambana ili kulinda nafasi yake kama ilivyokuwa msimu uliopita.

Cassilas ameanza kumtisha Mapunda baada ya kutua Simba akitokea Mtibwa Sugar ya Morogoro

Aliongeza kuwa kila mchezaji kwenye timu hana uhakika wa namba ndiyo maana wanapokuwa mazoezini wanajituma na kumshawishi kocha kuwapa nafasi.

"Casillas ni kipa bora msimu uliopita, hivyo ni mzuri na mimi nimejipanga kukabiliana na changamoto hiyo, pia naamini kila mmoja atahakikisha anamridhisha mwalimu," alisema kipa huyo.

Simba tayari imeshaanza kujifua kujiandaa na msimu mpya wa Ligi ya Bara na jana jioni Mcroatia, Zdravko Logarusic, alikiongoza kikosi chake kwa mara ya kwanza tangu arejee kutoka likizo kwenye Uwanja wa Chuo Kikuu Mlimani.

Hata hivyo Simba kama zilivyo timu nyingine zenye wachezaji katika timu ya Taifa (Taifa Stars) itawakosa nyota wake wa kikosi cha kwanza katika maandalizi.

Nyota hao ni pamoja na Amri Kiemba, Haroun Chanongo, Jonas Mkude, Ramadhani Singano 'Messi' na Joram Mgeveke walio katika kambi ya timu ya Taifa Stars wakati Amissi ambwe naye ameitwa kwenye timu ya taifa ya Burundi huku baadhi wakiwa bado hawajaripoti mazoezini akiwamo beki, Donald Musoti.

Simba ilimaliza msimu uliopita ikiwa katika nafasi ya nne na hivyo mwakani haitashiriki mashindano yoyote ya kimataifa wakati mabingwa ni Azam ambao watashiriki Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Kagame huku Yanga walioshika nafasi ya pili watapeperusha bendera ya Bara kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC