Ruka hadi kwenye maudhui makuu

GOTZE ASEMA, LILE LILIKUWA BAO LA NGEKEWA TU KWAKE.

Shujaa wa Ujerumani, Mario Gotze amesema kufunga bao pekee na la ushindi katika fainali ya Kombe la Dunia ni kama bahati na zawadi yake katika msimu wake mgumu akiwa Bayern Munich.

Gotze (22), mwenye sura ya kitoto, alituliza kifuani mpira wa krosi ya Andre Schuerrle kabla ya kupiga shuti kufunga bao katika dakika ya 113, na kuipa Ujerumani ushindi 1-0 dhidi ya Argentina kwenye Uwanja wa Maracana, Rio de Janeiro, Brazil.


“Ni hisia ambazo siwezi kuziamini wala kuzielezea,” alisema kiungo huyo wa Bayern.

“Sijui hata nilielezee vipi hili. Unajikuta unafunga bao na hujui kitu kitakachotokea. Itakuwa ni sherehe pamoja na timu nzima na taifa kwa ujumla.  Ni kama ndoto iliyotimia.”

Gotze aliingia kuchukua nafasi ya mkongwe Miroslav Klose kabla ya kuanza kwa muda wa nyongeza. Hilo ni bao lake la 11 kuifungia timu ya taifa katika michezo 35 aliyoitumikia miamba hiyo maarufu kama ‘Die Mannschaft’.

Alitwaa pia tuzo ya mchezaji bora wa mechi, ambayo alipewa uwanjani hapo wakati Ujerumani ikiweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza kutoka Bara la Ulaya kutwaa taji hilo katika ardhi ya bara la Amerika Kusini.

Gotze anaungana na ‘Der Bomber’ Gerd Mueller, ambaye alifunga bao la ushindi kwa Ujerumani Magharibi katika mchezo wa fainali 1974 mjini Munich, akiwa mchezaji mwingine wa Bayern kulipa ubingwa taifa hilo.

Gotze alitua nchini Brazil akiwa ametokea kwenye hali ngumu katika msimu wake wa kwanza na miamba hiyo ya Bavaria, akiwa ameshindwa kupata nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza cha kocha Pep Guardiola.

Akiwa ametwaa mataji mawili ya Bundesliga na Borussia Dortmund, klabu ambayo alijiunga nayo akiwa na miaka nane, Gotze alikuwa adui namba moja wa mashabiki wa Borussia Aprili 2013, alipokubali uhamisho wa Euro 37 milioni ili kujiunga na Bayern.

Uhamisho huo umemfanya nyota huyo kuipa kisogo timu iliyomkuza na ya nyumbani kwao. Alikuwa nje katika mchezo wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya Mei 2013, baada ya kuumia katika mchezo wa nusu fainali ya michuano hiyo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...