Ruka hadi kwenye maudhui makuu

UKICHEZA SIMBA AU YANGA NDIO UNACHAGULIWA TAIFA STARS- CASILAS

Na Prince Hoza

MLINDA lango wa kutumainiwa wa timu ya Mtibwa Sugar ya Manungu Turiani mkoani Morogoro Hussein Sharrif 'Cassilas' ambaye pia ndiye kipa bora wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara (2013/14) ameponda kauli zinazotolewa na wadau wa soka hasa baada ya yeye kutangazwa kipa bora.

'Mimi ndio kipa bora lakini siwezi kuitwa Stars labda niwe Simba, Yanga au Azam', anasema Casilas.


Casilas amelaani vikali baadhi ya wadau kuponda uteuzi wake wa kuwa kipa bora msimu uliomalizika wakati hayupo kwenye timu ya taifa, Taifa Stars.

Hivi karibuni mchambuzi wa soka na mdau maarufu Joseph Kanakomfumo amebeza uteuzi wake wa kuwa kipa bora wakati hayupo Stars, Kanakomfumo ameshangazwa na uteuzi huo na kudai imekuwa mara kwa mara kutoa tuzo kwa wasiostahili.

Lakini mlinda lango huyo ameipuuza kauli hiyo ya Kanakomfumo ambaye pia ni kocha kitaaluma, Casilas amedai kuwa kuna kasumba katika uteuzi wa timu ya taifa, Taifa Stars tena imeendelea kukithili.

Amesema ili uitwe timu ya taifa basi ni lazima uwe mchezaji wa Simba, Yanga au Azam fc, hivyo inawawia vigumu wachezaji kama wao kuonekana bora.'Nastahili kuwa kipa bora, lakini kuitwa kwenye timu ya taifa labda nichezee Simba, Yanga au Azam', alisema na kuongeza.

'Yamekuwa mazoea ya kuteua kikosi cha timu ya taifa kwa kufuata timu zenye majina makubwa ambazo ni Simba, Yanga na Azam fc, ila kama wangejali ubora wa mchezaji husika nasi wasingepata taabu kwani tupo kibao huku Mtibwa na kwingineko', aliongeza kipa huyo aliyelamba kitita cha shilingi Mil 5.

Kipa huyo ameponda uteuzi wa timu ya taifa ambaounatokana na majina na si uwezo wa mchezaji, na ndio maana maendeleo ya soka nchini yanadolola kutokana na uduni wa wachezaji.

Na ili timu ya taifa iungwe mkono na wengi basi ni bora wachezaji wakatokea Zimba, Yanga au Azam, kwani timu hizo tayari zimeota mizizi kwa mashabiki wengi wa soka nchini, Casilas anawaniwa vikali na Simba ingawa timu yake ya
Mtibwa imegoma kumuuza.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...