Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TAIFA STARS HAIKAMATIKI........

Timu ya soka ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) ilitinga hatua ya pili ya mchujo ya kuwania kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika 2015 kufuatia sare ya 2-2 ugenini iliyowapa ushindi wa jumla wa 3-2 dhidi ya Zimbabwe kwenye Uwanja wa Taifa jijini Harare jana.

Matokeo hayo yanamaanisha kwamba Stars sasa itaikabili Msumbiji ambayo iliing'oa Sudan Kusini kwa jumla ya mabao 5-0 katika mechi ya hatua ya pili ya mchujo itakayofanyika nyumbani wikiendi ya Julai 18-20 na ya marudiano ugenini Maputo wikiendi ya Agosti 1-3. Mshindi baina ya Stars na Msumbuji ataingia katika hatua ya makundi.


Endapo Tanzania itaitoa Msumbiji itaingia katika Kundi F la kufuzu ambalo linaundwa na timu za Zambia, Niger, Cape Verde.

Timu mbili kutoka kila kundi la kuwania kufuzu kati ya makundi saba yaliyopo, pamoja na mshindi wa tatu mmoja aliyefanya vizuri zaidi, wataungana na wenyeji Morocco kwa ajili ya fainali hizo za Mataifa ya Afrika 2015 nchini Morocco.

Stars jana ilianza vibaya mechi baada ya kujikuta ikitanguliwa kwa goli la mapema katika dakika ya 13 lililofungwa na Danny Phiri.

Hata hivyo, Stars ilicharuka na kusawazisha goli hilo dakika 13 baadaye lililofungwa na beki wa kati Nadir Haroub 'Cannavaro'.

Stars, ambayo katika mechi ya awali jijini Dar es Salaam iliifunga The Mighty Warriors 1-0 kwa bao la mshambuliaji wa Azam FC, John Bocco 'Adebayor', ilijiweka katika nafasi nzuri zaidi ya kusonga mbele katika michuano hiyo ya Afrika wakati mshambuliaji wa TP Mazembe, Thomas Ulimwengu alipoifungia goli la kuongoza katika dakika ya 46.

Hata hivyo, Zimbabwe walihitaji dakika tisa tu kusawazisha bao hilo kupitia kwa Katsande na kufanya dakika za mwisho za mechi hiyo kuwa ngumu kwa wageni wakati wenyeji wakisaka magoli mawili waliyohitaji ili kusonga mbele.

Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ilikwenda Msumbiji chini ya mkuu wa msafara Rais wa Shirikisho la Soka (TFF), Jamal Malinzi na ilipokewa na hisia za 'mizengwe' baada ya kudaiwa kunyimwa funguo za vyumba katika hoteli waliyofikia, kwa mujibu wa ripoti za kutoka nchini humo.

Kwa mujibu wa takwimu za mechi ya jana, Zimbabwe ilikaa na mpira kwa asilimia 52 dhidi ya asilimia 48 za Stars, Zimbabwe ilipia kona 5 dhidi ya 2 za Stars, huku pia wenyeji wakifanya majaribio ya kufunga 6 dhidi ya manne ya Stars.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC