Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MALINZI AIKATAKATA YANGA, APINGA MANJI KUONGEZEWA MWAKA MMOJA

Wakati Shirikisho la Soka nchini (TFF) likiwa halijapokea rasmi maamuzi ya kusogeza mbele Uchaguzi Mkuu wa Klabu ya Yanga, Rais wa shirikisho hilo, Jamal Malinzi, amesema katika uongozi wake hataruhusu kuona wanachama wanafanya maamuzi yaliyo kinyume na katiba za vyama na klabu zao.

Wanachama wa Yanga waliokutana Juni Mosi, mwaka huu katika mkutano wa marekebisho ya katiba, pia walikubaliana kusogeza mbele uchaguzi mkuu wa klabu hiyo hadi Juni 15, mwakani.


Hata hivyo, baadhi ya wanachama wa Yanga wakiongozwa na Juma Magoma mwenye kadi namba 2319, wamepinga maamuzi hayo na kumuandikia Malinzi barua ya kutaka asaidie klabu yao ifanye uchaguzi ndani ya siku 90 na ili katiba yao isivunjwe.

Akizungumza kwa njia ya simu kutoka nchini Brazil jana mchana, Malinzi, alisema bado hajaiona barua hiyo ya wanachama wa Yanga iliyondikwa tangu Juni 5, mwaka huu na kupelekwa katika ofisi ya kiongozi huyo.

Malinzi alisema licha ya kutoipata barua hiyo kutokana na yeye kuwa nje ya nchi, uongozi wake muda wote utahakikisha wanachama wake wanafuata taratibu, kanuni na katiba zao.

"Kuhusiana na barua ya wanachama wa Yanga siwezi kusema chochote, niko kwenye mikutano ya CAF/Fifa, sijaiona barua hiyo," alisema kwa kifupi Malinzi.

Wanachama hao katika barua yao walisema kuwa kuruhusu viongozi waliopo kuendelea kuwaongoza kwa kipindi cha mwaka mmoja ni kudhihirisha wazi wote hawaifahamu Katiba ya Yanga, TFF na Baraza la Michezo la Taifa (BMT).

Alisema kwa mujibu wa Katiba ya Yanga uongozi unapomaliza muda wake madarakani na kulazimika kuongezewa, wanatakiwa kuongezwa muda wa siku 90 na baada ya hapo kuitishwa uchaguzi mkuu na si vinginevyo.

Naye Goefrey Mwaipopo (2481), alisema wanashangaa kuona Mama Fatma Karume anaitwa mdhamini wakati jina lake haliko kwenye orodha ya wadhamini wa klabu hiyo.

Viongozi wa Yanga ambao wanamaliza muda wao kikatiba wa miaka minne waliingia madarakani katika uchaguzi uliofanyika mwaka 2010, hivyo kwa kauli hiyo ya Malinzi kama ataitekeleza ni wazi Yanga watalazimika kufanya uchaguzi baada ya siku 90 na si mwakani kama walivyopitisha katika mkutano mkuu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC