Ruka hadi kwenye maudhui makuu

WAMBURA, KABURU KUENGULIWA UCHAGUZI MKUU SIMBA

Michael Wambura na Geofrey Nyange ‘Kaburu’ pamoja na wagombea  wa ujumbe wa kamati ya utendaji ya Simba wamewekewa pingamizi la kuwania uongozi.

Mwanachama Swaleh Madjapa kadi namba 00574, Mwinyi Dossy kadi namba 564 pamoja na kocha wa zamani wa timu hiyo, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ ndio waliojitokeza jana kuweka pingamizi kwa wagombea hao.


Mbali na Wambura na Kaburu,  wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba, Swedi Nkwabi, Said Pamba, Ibrahimu ‘Maestro’, Joseph Itang’are ‘Kinesi’ na Daniel Manembe wamewekewa pingamizi na wanachama watatu tofauti kwa madai ya kukiuka katiba ya Simba.

Madjapa alimwekea pingamizi  Wambura akidai wakati akichukua fomu alifanya kampeni kinyume na taratibu na kwamba ana vielelezo vyote vinavyothibitisha kuwa Wambura alifanya kampeni kabla ya muda wake.

Wambura aliwahi kuwa mwenyekiti wa klabu hiyo, lakini akasimamishwa na uongozi baada ya kufungua kesi mahakamani kupinga kuenguliwa kwenye uchaguzi mwaka 2008, kitendo ambacho ni uvunjaji wa katiba.

Pia aliwawekea pingamizi wagombea wote ambao ni wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba inayomaliza muda wake kwa kile alichoeleza kuwa kwa kipindi cha miaka minne walichokaa madarakani hakuna walichofanya cha maana kinachofanya waombe tena kupewa miaka mingine minne ili wamalizie, zaidi ya vurugu.

Naye Kihwelo, anayegombea nafasi ya makamu wa rais, aliwekea pingamizi Kamati ya Utendaji kwa kile alichodai walikiuka katiba kwa kuendesha vikao visivyo halali na kuupindua uongozi wa  Ismail Aden Rage na pia walikiuka katiba ya klabu hiyo kwa kutojaza nafasi ya makamu mwenyekiti iliyoachwa na Geofrey Nyange ‘Kaburu’ ndani ya siku 90.

Pia, wajumbe hao wa kamati ya utendaji inayomaliza muda wake waliwekewa pingamizi na Mwinyi Dossy kadi namba 564.

Kaburu aliwekewa pingamizi na mchezaji wa zamani wa klabu hiyo, Athurh Mwambeta (kadi namba 01005) ambaye pia amewekewa na Swedi Nkwabi. Mwambeta amedai Kaburu akiwa makamu mwenyekiti alikiuka katiba ya Simba ibara ya 33 (5) na 28 (1b) kwa kushindwa kuwasilisha ripoti ya mapato na matumizi ya fedha katika mkutano mkuu mwaka 2010 hadi mwaka 2013 alipojiuzulu.

Pia, alidai kuwa kwa mujibu wa katiba ya Simba kiongozi anayejiuzulu haruhusiwi kugombea tena uongozi ndani ya klabu hiyo kwa vipindi vitatu na kudai kuwa Kaburu hajafikisha vipindi vitatu toka ajiuzulu.

Kwa upande wa pingamizi la Nkwabi, Mwambeta alidai kuwa alikiuka katiba wakati wa uongozi wao kwa kuendesha mapinduzi ya kumpindua Rage. Swedi pia aliwekewa pingamizi na Lucas Mbapila kwa madai ya kukiuka kanuni za uchaguzi.

Chano Almas aliwekewa pingamizi Dossy na Madjapa kwa madai ya kukiuka katiba.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC