Ruka hadi kwenye maudhui makuu

RIO FERDINAND ALIVYOTEMWA 'KIROHO MBAYA' MAN UNITED

BEKI Rio Ferdinand amemaliza maisha take ya soka Manchester United baada ya kuambiwa hatapewa Mkataba mpya.
 
Mkuu wa Old Trafford, Ed Woodward alimpa habari hizo za kusikitisha Ferdinand mwenye umri wa miaka 35 katika chumba cha kubadilishia nguo Jumapili wakati wa mchezo wa mwisho na Southampton. 
 
Wengi wamesikitishwa na kitendo cha Woodward kuamua kumuacha 'kiroho mbaya' Ferdinand baada ya miaka 12 ya kuitumikia klabu hiyo kwa moyo wake wote.

Champions: Ferdinand shows off the 2006/07 Premier League trophy with Cristiano Ronaldo
Kumbukumbu za furaha: Ferdinand akiwa ameshika taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka 2008 na Cristiano Ronaldo baada ya kuifunga Chelsea kwa penalti
New boy: Ferdinand shows off his United shirt with then manager Sir Alex Ferguson after joining from Leeds for £29.1million in July, 2002
Alipowasili: Ferdinand akikabidhiwa jezi ya United na mocha wakati huo, Sir Alex Ferguson baada ya kujiunga na timu hiyo akitokea Leeds kwa dau la uhamisho la Pauni Milioni 29.1 Julai mwaka 2002

FERDINAND MAN UNITED

Kusajiliwa: July 2, 2002
Ada: Pauni Milioni 29.1
Mechi alizocheza: 455
Mabao aliyofunga: 8
Mataji aliyoshinda: Ligi Kuu (2002/03, 2006/07, 2007/08, 2008/09, 2010/11, 2012/13), Ligi ya Mabingwa (2007/08), Kombe la Ligi (2005/06, 2008/09), Kombe la Dunia la Klabu (2008)
Katika taarifa aliyoweka kwenye tovuti yake binafsi usiku wa jana, Ferdinand amesema; "Mambo fulani yamenifanya nishindwe kusema kwaheri kwa namna amabyo ningependa,".
Na huku akiwa amekubali kumruhusu beki mwingine wa kati Nemanja Vidic kuondoka, mchezaji mwenzake wa zamani Ferdinand, Gary Neville ametweet: "Hivyo inaonekana kama Rio na Vida wameruhusiwa kuondoka!!!
Beki huyo wa zamani wa England amewaambia wenzake safe ya 1-1 juzi ndiyo ilikuwa mechi yake ya mwisho katika klabu hiyo wakiwa kwenye ndege kurejea kutoka St Mary na akawaomba wamsainie mpira abaki nao kama kumbukumbu yake.
Ferdinand, ambaye alikuwa mchezaji ghali kihistoria England wakati anasajiliwa United kutoka Leeds kwa dau la Pauni Milioni 29.1 Julai mwaka 2002, ameichezea timu hiyo mechi 455 lakini alionekana hafai chini ya David Moyes.
Hard man: Ferdinand is escorted from the pitch by Robin van Persie after being cut by a coin thrown from the crowd during a Manchester derby in 2012
Amemwaga damu: Ferdinand akisindikizwa kutoka uwanjani na Robin van Persie baada ya kuchanwa na sarafu iliyorushwa uwanjani na mashabiki wakati wa mechi ya mahasimu wa Jiji la Manchester mwaka 2012
On target: Ferdinand scores a rare goal against Liverpool in a 2-0 win at Old Trafford in 2006
Alikuwa anafunga pia: Ferdinand akifunga boa dhidi ya Liverpool katika ushindi wa 2-0 Uwanja wa Old Trafford mwaka 2006

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC