Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAKALA: TAKUKURU KUWENI MAKINI UCHAGUZI MKUU SIMBA

Na Prince Hoza

NATOA angalizo kwa taasisi ya kupambana na rushwa nchini Takukuru kuwa macho na uchaguzi wa klabu ya Simba unaotarajia kufanyika mwishoni mwa mwezi huu.

Tayari uchaguzi huo umeonyesha kuwepo kwa vitendo vya rushwa vinavyodaiwa kufanywa na baadhi ya wagombea, wapo baadhi ya wagombea wamekuwa wakitumia kuwapa wanachama fedha ili wawachague.


Lakini pia wapo wagombea wanaotoa rushwa kwa njia ya kuahidi kufanya usajili wa kutisha ama kumleta nyota fulani katiika klabu hiyo ili mradi akubalike kwa wanachama.

Takukuru kama hamjakuwa makini basi vitendo vya rushwa vitazidi kushamili hapa nchini, aidha pia baadhi ya wagombea wamekuwa wakitoa fedha kwa wanachama wa klabu hiyo kupitia matawi yao na kuwaahidi kuwajengea mazingira safi pindi tu akiingia madarakani.

Aina hii ya rushwa imezoeleka kwenye vilabu vyetu vya soka hasa Simba na Yanga lakini sasa imezidi kukua. njia bora na nafuu ni kuiteketeza kwa nguvu zote, sifurahishwi na baadhi ya wagombea ambao wameingia katika kinyang'anyiro hicho kwa maana ya kushinda na kwa sera na wenzao.

Badala ya kushindana kwa sera wamekuwa wakitumia nafasi nyingine ya kugawa fedha kwa wanachama hasa wale wenye njaa huku wakidiriki kuwaponda wagombea wenzao.

Nawaambia wanachama wa Simba msikubali kurubuniwa kwa fedha kidogo wala usimuone mgombea mwenye fedha ndito anafaa kuiongoza Simba, Simba ni mali ya watu wote iwe masikini au tajiri.

Unapokubali kununuliwa kwa fedha ina maana umeiweka shakani klabu yako kwa kipindi chote cha utawala wa kiongozi aliyekununua, pia hautaweza kumpinga kwa lolote hata kama anaboronga kwa vile umenunuliwa.

Na iweje uwe mtumwa kwenye klabu yako wakati hata wewe ulipaswa kugombea? umefika wakati tuachane na wagombea wanaoingia kwa lengo la kutoa fedha kama njugu, kama kiongozi ni tajiri wa fedha alikuwa wapi wakati Simba ilipotangaza kujenga uwanja Bunju kwa siku 100.

Wanachama waliandamana kwa majembe, shoka, nyundo, panga nk kufyeka uwanja wakati kumbe kuna matajiri wamejificha pembeni wanangoja uchaguzi, viongozi wa namna hii hawafai na tuwaogope kama ukoma.

Nakumbuka kauli ya baba wa taifa hayati Julius Kambarage Nyerere alisema 'Ikulu hakununuliwi' hiyo ina maana mgombea anayetaka kuongoza Simba kwa kutoa fedha hafai..tuonane wiki ijayo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC