Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAKALA: ETI HII NDIO TIMU YA MWISHO DUNIANI KWA UBORA WA KANDANDA!

Nicky Salapu ,kipa aliyeshiriki mechi waliofungwa 31-0 na Australia
Mwaka wa 2001 timu ya Australia iliandikisha rekodi ya kufunga mabao mengi zaidi katika kandanda ya kimataifa .

Australia ilifunga Samoa mabao 31 kwa nunge .
Mshambulizi wa Australia Archie Thompson,vilevile aliiingia katika daftari za kumbukumbu kama mfungaji mabao mengi zaidi katika mechi ya kimataifa alipofunga mabao 13.


Mvua hiyo ya mabao iliipelekea American Samoa kushuka ngazi na kujikita katika nafasi ya mwisho ya orodha ya mataifa yanayocheza kandanda ya kimataifa kwa zaidi ya miaka 10.
Serikali,ya taifa hilo ilichukua jukumu la kumtafuta kocha mpya ilikuhakikisha timu hiyo inafuzu kwa kombe la dunia litakaloaanza mwezi ujao mjini Rio Brazil .

Kocha Mpya

Mjerumani Thomas Rongen ndiye aliyekabiliwa jukumu la kufufua hadhi ya kandanda katika kisiwa hicho mbali na kukomesha msururu wa matokeo duni na kushindwa katika kila mechi waliocheza ya kimataifa .
Kocha huyo alianza kwa kuwasaili wachezaji wliokuwepo katika mechi hiyo ya kihistoria huku akifahamu kuwa matamanio ya takriban wasamoa eflu 65 yalikuwa mabegani mwake .
Kocha mjerumani Thomas Rongen aliyeifufua timu ya Samoa
Aidha moyo wa wachezaji na motisha waliokuwa nao ilimshangaza kocha Rongen.
''Itakuwaje mtu anawania kuiwakilisha taifa lake katika kikosi ambacho kimeshindwa katika mechi zote ?''
Kiungo Jaiyah Saelua aliyeshiriki katika mechi hiyo alisema hata ingawa hawakuwa na viwango vya ushindani kama wachezaji wapinzani wao ilikuwa jambo la kujivunia kuvalia jezi la taifa.

Kila mtu alimshauri kocha huyo anayeishi marekani dhidi ya kuchukua wadhfa huo kwani ingemletea fedheha.
Hata mkewe alimzomea kuwa punguani endapo atachukua hatamu American Samoa.
Timu ya taifa ya Samoa
Lakini Mjerumani huyo alitua Samoa kwa kishindo na kuanza kazi na wachezaji waliokuwepo huko akiwemo mwanamke Jaiyah Saelua, aliyezaliwa kama mwanaume akiitwa Johnny,lakini maumbile yake yakabadilika na kuwa ya kike.

Kwa ufupi mwaka mmoja tangu hapo Novemba 2011, American Samoa ilisajili ushindi wake wa kwanza katika historia yake kwa kuandikisha ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Tonga.
Ushindi huo ulikuwa wa kwanza baada ya kushindwa katika mechi 30 zilizochezwa katika kipindi cha miaka 20.

Kocha Thomas Rongen aliongoza timu hiyo kusherekea ni kama walioshinda kombe la dunia akisema kuwa hiyo kwa hakika ilikuwa ni historia .
Timu hiyo ilijizolea pointi 18 na ikaimarika hadi nafasi ya 197 kati ya mataifa 209 yanayoorodheshwa na shirikisho la soka duniani FIFA.

Nafasi ya mwisho 207 inashikiliwa kwa pamoja kati ya mataifa matatu Bhutan ,San Marino na visiwa vya Turks & Caicos .

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC