Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUMEKUCHA ULAYA LEO, ATLETICO MADRID V REAL MADRID

‘MWALI’ wa Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka huu anatarajiwa kumpata mwenyewe usiku wa leo katika fainali itakayopigwa Uwanja wa Luz mjini Lisbon, Ureno baina ya Real Madrid na Atletico Madrid za Hispania.

Huo ni mchezo wa kuhitimisha msimu wa 59 wa michuano hiyo mikubwa zaidi ya klabu Ulaya na msimu wa 22 tangu michuano hiyo ianze kutumia jina hilo kutoka Klabu Bingwa ya Ulaya.
Hii itakuwa mara ya kwanza katika historia ya michuano hiyo kukutanisha timu kutoka Jiji moja, Madrid.


Ikumbukwe mshindi wa mechi hiyo atakutana na  Sevilla, pia ya Hispania mabingwa wa michuano ya pili kwa ukubwa ya UEFA, Europa League katika mechi ya Super Cup ya UEFA.
Na pia ataingia moja kwa moja Nusu Fainali ya Klabu Bingwa ya Dunia ya FIFA mwaka huu.

Real Madrid ndiyo klabu yenye mafanikio zaidi katika Ligi ya Mabingwa, ikiwa imetwaa mataji tisa.

Hispania kwa ujumla ndiyo inaongoza kutoa mabingwa wengi wa michuano hiyo, hadi sasa ikitoa mabingwa 13, ikifuatiwa na England na Italia ambazo kila moja imetoa mabingwa 12.

Jumla ya klabu 22 tofauti zimekwishatwaa taji hilo, kati ya hizo 12 zimeshinda Kombe hilo zaidi ya mara moja na tangu michuano hiyo ibadilishwe jina na muundo wake mwaka 1992, hakuna timu iliyoweza kubeba ‘mwali’ mfululizo.

AC Milan ndiyo ilikuwa timu ya mwisho kutetea taji hilo msimu wa 1989–1990 na Bayern Munich, waliokuwa mabingwa watetezi baada ya kuifunga Borussia Dortmund 2-1 katika fainali mwaka jana, walitolewa katika Nusu Fainali na Real Madrid mwaka huu.

Bingwa wa michuano hiyo anatarajiwa kujinyakulia kitita cha Euro Milioni 10.5 na mshindi wa pili Euro Milioni 6.5 wakati timu zilizotolewa katika Nusu Fainali, Beyern na Barcelona kila moja itapata Euro Milioni 4.9.

UEFA pia hutoa Euro Miloni 2.1 kwa kila timu inayofuzu kwenye Raundi ya awali ya michuano hiyo, Euro Milioni 8.6 kwa zinazoingia hatua ya makundi, wakati timu inayoshinda mechi katika hatua hiyo inapata Euro Milioni 1 na sare Euro 500,000.

Timu zinazongia kwenye hatua ya 16 Bora inapata Euro Milioni 3.5 wakati kwa zinazofuzu Robo Fainali zinapata Euro Milioni 3.9.

Wakati Real ina mataji tisa iliyoyatwaa misimu ya
1956, 1957, 1958, 1959, 1960, 1966, 1998, 2000 na 2002 pamoja na kushika nafasi ya pili mara tatu 1962, 1964 na 1981, Atletico Madrid iliingia fainali mara moja tu mwaka 1974 na kufungwa na Bayern Munich.

Nyota wa Real, Cristiano Ronaldo na Gareth Bale waliokuwa majeruhi wote wamepona na wamekuja na timu yao Lisbon tayari kwa kuipigania kupata taji la 10 la michuaho hiyo.

Mshambuliaji tegemeo wa Atletico Madrid, Diego Costa ambaye ni majeruhi pia mapema wiki hii alipelekwa Serbia kutibiwa na mganga wa kienyeji ili aweze kupona haraka na kucheza.    
Atletico tayari wameshinda ubingwa wa Ligi Kuu ya Hispania msimu huu ikiwazidi kete vigogo wa nchi hiyo Barcelona siku ya mwisho walipotoa nao sare ya 1-1 na Real baada ya kukosa taji la La Liga watakuwa wanajaribu kurejesha heshima katika Ligi ya Mabingwa.
 
Tangu juzi, Jiji la Lisbon limetawaliwa na shamrashamra za mashabiki wa Real na Atletico waliosafiri kutoka Madrid kuja kuzisapoti timu zao.

Gwiji wa zamani wa Real, Mreno Luis Figo ndiye balozi wa mchezo huo ambaye baadaye anatarajiwa kuwamo katika kikosi cha magwiji wa timu hiyo kitakachofanya ziara Tanzania Agosti mwaka huu.

Wapenzi wa soka kutoka nchi mbalimbali duniani nao pia wapo hapa wakiwemo Watanzania. Je, ni Real au Atletico atampandisha ndege mwali wa Ligi ya Mabingwa kurejea naye Madrid? Bila shaka hilo ni jambo la kusubiri na kuona.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC