Ruka hadi kwenye maudhui makuu

JULIO AMTUNISHIA KIFUA KABURU, AMUAMBIA “TUNAOMBA PENZI KWA DEMU MMOJA, MWENYE BAHATI YAKE ATABEBA TOTOZ”

KOCHA wa Mwadui FC ya Shinyanga, Jamhuri Kihwelu 'Julio' amekifafananisha kitendo cha kuwania uongozi katika klabu ya Simba na maamuzi ya mwanaume kumtongoza mwanamke.

Akichukua fomu kwenye ofisi za makao makuu ya Simba mjini Dar es Salaam jana kuwania Umakamu wa Rais wa Simba katika uchaguzi mkuu wa klabu hiyo utakaofanyika Juni 29 mwaka huu, Julio amesema kuwania uongozi wa Simba kunafanana sana na kumtongoza mwanamke.
Nipeni mimi; Julio akiwahutubia wanachama wa Simba SC alipokwenda kuchukua fomu jana na chini ni mpinzani wake Kaburu

Julio atawania nafasi hiyo dhidi ya viongozi waliomaliza muda wao, Geoffrey Nyange
‘Kaburu’, Joseph Itang’are ‘Kinesi’ na Swedi Nkwabi- ambao walikuwa mabosi wake alipokuwa kocha wa timu hiyo.
"Nimeamua kuwania uongozi ndani ya klabu ya Simba kwa sababu nina haki ya kikatiba ya kugombea nafasi yoyote. Kugombea uongozi Simba ni sawa na kutongoza mwanamke kwani hata kama akikubali utapata sifa na akikataa unapata sifa vile vile," alisema Julio.
Kessy Kikoti naye alirejesha fomu 
Aidha, Julio, licha ya kuiongoza Mwadui FC kumaliza nafasi ya pili katika Kundi C la michuano ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu huu, amesema bado anatambua kuwa yeye ni kocha halali wa Simba kwa sababu "kikao kilichowafukuzisha kazi kilikuwa batili na ndiyo maana Shirikisho la Soka nchini (TFF) liliyakataa mapinduzi na kumrudisha mwenyekiti wao Ismail Aden Rage madarakani."

"Kwa watu wenye kuona mbali ninaamini watanipa kura Simba kwa sababu mimi ni kocha pekee niliyekuwa ninakubali kufundisha Simba bila kulipwa mshahara na sasa ninaudai uongozi wa Dalali Sh. milioni 24 na nilikubali kupoteza hadi gari langu kwa ajili ya Simba," amesema zaidi Julio ambaye baadaye alasiri amewahutubia kwa dakika chache wapenzi wa Simba waliojitokeza kumsindikiza kuchukua fomu.

Akiwa msaidizi wa aliyekuwa kocha mkuu wa Simba, Abdallah 'King' Kibadeni, Julio na nyota huyo wa zamani mwenye rekodi pekee ya kufunga magoli matatu pekee yake katika mechi ya watani wa jadi, Simba na Yanga, walitimuliwa baada ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu huu baada ya kuitishwa kwa kikao batili cha Kamati ya Utendaji ya Simba ambacho Rage hakuhudhuria.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...