Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BAADA YA KUFUNGWA NA REAL MADRID, ATLETICO YAZUIWA NYOTA WAKE WOTE KUHAMA

KLABU ya Atletico Madrid itapambana kuhakikisha wachezaji wake bora na inatumai kwa umuhimu wao katika klabu na kwa kocha wao, Diego Simeone itasaidia wakibaki.

Kipa wa Chelsea anayecheza kwao kwa mkopo, Thibaut Courtois amezungumzia mustakabali wake baada ya kufungwa Real Madrid 4-1 katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, lakini kwa kiasi kikubwa hayuko mikononi mwa Atletico.

"Sina mawasiliano ya moja kwa moja na Chelsea,"amesema kipa huyo mwenye umri wa miaka 22, Courtois. "Sina lolote dhidi yao. Ni kwamba nina dhamana hii na Atletico, baada ya yote nimeishi na klabu hii kwa misimu mitatu iliyopita,".


"Ikiwa nitatakiwa kurudi Chelsea tu kwa ajili ya kucheza mechi za Kombe la FA na Kombe la Ligi, nitaangalia mazingira," amesema.

Mtendaji Mkuu wa Atletico, Miguel Angel Gil Marin, amesema kwamba Diego Costa atauzwa iwapo tu atataka mwenyewe kuondoka.

Gil amesema: "Tutajaribu kuhakikisha kwamba wachezaji wore muhimu wanabaki hapa. Tumezungumza vizuri sana na Diego abaci na tunataka kutimiza ndoto hii, lakini itategemea na yeye mwenyewe,".

"Lengo letu ni kutouza mchezaji yeyote labda yule ambaye ataomba mwenyewe kuuzwa. Kwa sababu ya mafanikio yeti katika Ligi ya Mabingwa, tuna fedha maana yake hatuhitaji kuuza mchezaji,"amesema.


Kiungo Koke na beki wa kushoto, Filipe Luis ni wachezaji winging wanaozitoa udenda klabu za Ligi Kuu ya England.

Lakini Koke ni kipenzi cha klabu hiyo na Filipe Luis na rafiki wa kocha Simeone, hali ambayo inaweza kuwafanya wabaki.

Simeone amesema: "Tutakuwa na mapumziko ya kutosha, kuangalia Kombe la Dunia na kisha tutarejea kutetea ubingwa wetu wa Ligi,".

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...