Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TIMU YA WANAWAKE YA LIVERPOOL MBIONI KUTWAA UBINGWA UINGEREZA

SIYO kaka zao tu wanaotesa Uingereza, Timu ya wanawake ya Liverpool inayofahamika kwa jina la Liverpool Ladies hivi karibuni imeanza kujiimarisha kiulinzi ili kutwaa kombe la The FA Women's Super League.

Timu hiyo ambayo inakabiliwa na mechi kali zidi ya wageni wao Man city Ladies inayotarajiwa kuchezwa kesho tar 17 ambapo Liverpool Ladies watakuwa wenyeji.


Timu za Liverpool ya upande wa kike na kiume zimekuwa zikitikisa michuano inayoendelea huko Uingereza ambapo mpaka sasa timu ya wanawake ya Liverpool inaongoza kwa alama 36 ambapo imeshacheza mechi 14  ikifuatiwa na timu ya wanawake ya Bristol Academy Ladies ikiwa na alama 31 nao pia mpaka sasa wameshacheza mechi 14.

Timu ya wanawake ya Arsenal imeshika nafasi ya tatu kwa alama 30 huku ikiwa imeshacheza mechi 14  vile vile timu ya wanawake ya Birmingham City ikishika nafasi ya nne kwa alama 18 huku ikiwa imesha cheza mechi 14 .

Kwa upande wa Liverpool sasa mambo safi kwa kuwa timu zote zipo vizuri kwa wanaume na wanawake pia mpaka sasa Primier League inaongozwa na timu ya Liverpool yenye alama 77 mabayo imeshacheza mechi 34 naChelsea ikishika nafasi ya pili kwa alama 75 pia imeshacheza mechi 34.

Man city ikiambulia kuwa nafasi ya tatu kwa alama 70 amabayo mpaka sasa imeshacheza mechi 32 timu ya Everton imeshika nafasi ya nne kwa alama 66 ambayo imeshacheza mechi 33.

Timu ya wanawake ya Liverpool inakabiliwa na mechi ngumu hivi karibu ikisha cheza na Man City alhamis hii itacheza na timu ya wanawake ya Chelsea jumapili tar 20 ambapo Chelsea Ladies watakuwa ni wenyeji.

Timu ya Liverpool Ladies inaongozwa na wachezaji machachari wanaoongoza kwa kufunga magori kama mchezaji Natasha Dowie ambaye msimu uliopita alifunga mabao 13 na kuwa mfungaji bora wa kike pia Natasha Dowie alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa kike wa mwaka 2013.

Mpaka sasa hakuna timu ya wanawake ambayo inaweza ikaipokonya Liverpool nafasi ya kwanza asilimia kubwa wote wameshacheza mechi 14.

Liverpool Ladies imeipita alama 5 Bristol Academy Ladies ambayo inashikilia nafasi ya pili huku ikiiacha kwa alama 6 timu ya Arsenal Ladies ambayo inashikilia nafasi ya 3.

Kulingana na viwango vya wachezaji wa Liverpool hakuna timu ambayo inaweza ikaipiku Liverpool kwa asilimia mia na hata kama ikitokea itakuwa imefanya kazi ya ziada.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC