Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA KWENDA Z,BAR LEO, YANGA YAAPA KUTOFUNGWA TENA NA SIMBA

Wakati  timu ya Simba itaenda mjini Zanzibar leo kwa ajili ya kuanza kambi ya kuwakabili Yanga, mahasimu wao hao wa jadi wamesema timu yao kamwe haitafungwa kizembe tena kama ilivyokuwa katika mechi yao iliyopita.

Yanga ilifungwa kizembe 3-1 dhidi ya Simba katika mechi ya 'Nani Mtani Jembe' kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Desemba 21, mwaka jana, mechi ya 'ndondo' iliyowafukuzisha kazi makocha Ernie Brandts raia wa Uholanzi na mzawa Felix Minziro.


Akizungumza jijini hapa mara tu baada ya mechi yao ya raundi ya 25 ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara walioshinda 2-1 dhidi ya Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini hapa juzi, kocha msaidizi wa Yanga, Boniface Mkwasa alisema hawako tayari kuona tena timu yao inafungwa magoli ya kizembe na Simba katika mechi yao ya mwisho dhidi ya Simba msimu huu kwenye Uwanja wa Taifa Jumapili.

"Tumekosa ubingwa lakini hatuko tayari kufungwa kizembe na Simba katika mechi ya mwisho," alisema Mkwasa.

Naye kocha wa Simba, Mcroatia Zdravko Logarusic alisema jana kuwa anaondoka na wachezaji wote kwa ajili ya kambi hiyo ya mjini Zanzibar.

Loga ambaye ameishuhudia timu yake ikiyumba katika msimu mbaya ambao imefungwa mechi sita na kutoka sare 10 katika mechi zao 25 za msimu huu hadi sasa, amesema atahakikisha anaifunga Yanga ili kumaliza msimu kwa heshima.

Simba iko katika nafasi ya nne ya msimamo wa Ligi hiyo ambayo imeshampata bingwa wake mpya Azam FC aliyeutwaa bila ya kupoteza mechi.

Yanga wamejihakikishia kumaliza katika nafasi ya pili na ya mwisho ya kuiwakilisha nchi katika michuano ya kimataifa na itashiriki Kombe la Shirikisho.

Simba yenye pointi 37 bado haijawa na uhakika wa kumaliza katika nafasi ya nne kwani kipigo Jumamosi na ushindi kwa Ruvu Shooting iliyo chini yake kwa pointi 35 vitawashuhudia Wekundu wa Msimbazi wakimaliza katika nafasi ya tano.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...