Ruka hadi kwenye maudhui makuu

REAL MADRID WATWAA UBINGWA WA COPA DEL REY

Bale asherekea bao la ushindi dhidi ya Barcelona
Timu ya Real Madrid ndio mabingwa wa mwaka huu wa kombe la Copa del Rey .
Madrid waliwacharaza wapinzani wao wa jadi katika ligi ya nyumbani La liga Barcelona mabao 2 kwa 1 katika fainali iliyochezwa jana mbele ya mfalme wa Uhispania .


Kocha wa Madrid Carlo Ancelotti alikuwa anajikuna kichwa kwani mshambulizi wake nyota Cristiano Ronaldo hakuwa uwanjani kutokana na jeraha la mguu na hivyo ikambidi kumchezesha mshambulizi aliyegharimu kitita kikubwa zaidi msimu huu Gareth Bale .

Na alidhibitisha udedea wake alipofuma bao la ushindi zikiwa zimesalia dakika tano tu mechi hiyo kukamilika na hivyo kuisadia kutwaa taji lake la 19 la Kombe hilo la mfalme la Copa del rey.
Real Madrid ilidhibitisha niya yao mapema kwa bao la dakika ya 11 Angel Di Maria .
Real Madrid yasherekea ushindi dhidi ya Barcelona
Lakini ikasawazishwa na bao la Bartra katikadakika ya 68 ya kipindi cha pili.
Bao la ushindi lilifungwa na Gareth Bale dakika tano tu kabla ya mechi hiyo kukamilika .
Bale alitimuka mbio na kumpiku mlinzi wa Barca Marc Bartra katikati ya kiwanja na akafululiza hadi akampiga chenga kipa machachari Jose Manuel Pinto na kuihakikishia Madrid ushindi.

Real Madrid bado iko mbioni kuwania kombe la ligi ya Uhispania, ambapo inashikilia nafasi ya pili na alama 79 alama tatu nyuma ya wakinzani wao Athletico Madrid.

Barcelona ambayo imekuwa ikishuhudia msururu wa matokeo yasiyo ya kuridhisha katika siku za hivi punde inafunga orodha ya tatu bora ikiwa na alama 78.

Madrid sasa inamuda wa kutoka kujiandaa kwa mechi ya nusu fainali ya kombe la mabingwa barani Ulaya dhidi ya mabingwa watetezi Bayern Munich ya Ujerumani.
Mechi nyingine ya nusu fainali ya kombe la mabingwa barani Ulaya itakuwa kati ya Chelsea ya Uingereza dhidi ya Atletico Madrid.

Nusu fainali hizo zitachezwa juma lijalo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC