Ruka hadi kwenye maudhui makuu

RATIBA KAMILI YA MATAIFA AFRIKA 2015


Droo ya Afcon2015 yatangazwa
Droo ya Kufuzu kwa kombe la mataifa Afrika mwakani{ Afcon} imefanyika huko cairo Misri huku timu zote za kanda ya Afrika Mashariki zikiratibiwa kucheza katika mechi za mchujo kabla ya kushirikimechi za kufuzu .


Kenya itachuana dhidi ya Visiwa vya Comoro ,Tanzania ipambane na Zimbabwe, Uganda imeratibiwa kutoana kijasho dhidi ya Madagascar nayo Rwanda ikivaana na Libya.

Raundi ya Kwanza

  • Liberia v Lesotho
  • Kenya v Comoros Islands
  • Madagascar v Uganda
  • Mauritania v Equatorial Guinea
  • Namibia v Congo
  • Libya v Rwanda
  • Burundi v Botswana
  • Central African Republic v Guinea Bissau
  • Swaziland v Sierra Leone
  • Gambia v Seychelles
  • Sao Tome e Principe v Benin
  • Malawi v Chad
  • Tanzania v Zimbabwe
  • Mozambique v South Sudan
Burundi kwa upande wake itachuana dhidi ya Botswana, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ikiratibiwa kuvaana na Namibia.
Baada ya kushiriki mkondo wa kwanza wa maondoano mataifa hayo tena yatalazimika kuchuana miongoni mwao ilikufuzu kwa awamu ya pili .
Mshindi wa mkondo huo wa pili ndio watakaojumuishwa katika makundi saba yaliyotajwa jana.

Raundi ya Pili

Liberia or Lesotho v Kenya or Comoros Islands
Madagascar ,Uganda v Mauritania ,Equatorial Guinea
Namibia , Congo v Libya , Rwanda
Burundi , Botswana v CAR , Guinea Bissau
Swaziland or Sierra Leone v Gambia , Seychelles
Sao Tome e Principe or Benin v Malawi , Chad
Tanzania , Zimbabwe v Msumbiji , Sudan kusini
Mechi za raundi ya kwanza zitangoa nanga tarehe 6-18 Mei.
Mechi za marudio zitasakatwa wikiendi ya tarehe 30-31 Mei hadi Juni Mosi .
Katika mechi zitakazoibua hisia ni pamoja na mabingwa watetezi Nigeria ambao wameratibiwa kuvaana na Afrika Kusini.
Mahasimu wa jadi kaskazini mwa Afrika Tunisia na Misri wameratibiwa kukwaruzana nayo Ghana,ikitoana kijasho na Togo.
Aidha Ivory Coast itafungua kampeini yake ya kufuzu kwa dimba hilo lenye hadhi barani dhidi ya mahasimu wao wakuu Cameroon.
Droo ya Makundi:
Kundi A :
Nigeria,
Sudan,
South Africa
{Namibia vs Congo Brazzaville/Libya vs Rwanda}
Kundi B :
Mali,
Ethiopia,
Algeria
{ Sao Tome e Principe vs Benin/Malawi vs Chad}
Kundi C:
Burkina Faso,
Gabon,
Angola
{ Liberia vs Lesotho/Kenya vs Comoros Islands}
Kundi D:
Ivory Coast,
Democratic Republic of Congo,
Cameroon
{ Swaziland vs Sierra Leone/Gambia vs. Seychelles}
Kundi E:
Ghana,
Guinea,
Togo
{Madagascar vs Uganda/Mauritania vs Equatorial Guinea}
Group F:
Zambia,
Niger,
Cape Verde Islands
{ Tanzania vs Zimbabwe/Mozambique vs South Sudan}
Kundi G:
Tunisia,
Senegal,
Egypt
{ Burundi vs Botswana/ Central African Republic vs Guinea Bissau}
Mechi za makundi zitaandaliwa kati ya tarehe 5-6 Septemba na tarehe 10 Septemba.
Mkondo wa pili utaandaliwa kati ya tarehe 14-15 November na 19 November.
Washindi wawili katika kila kundi watajiunga na wenyeji Morocco mwakani kwenye kipute cha kuwania taji la taifa bingwa barani Afrika 2015.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC