Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NI KIAMA LEO: REAL MADRID V BAYERN MUNICH


Munich, Ujerumani. Mabingwa watetezi Bayern Munich leo watakuwa na kazi kubwa ya kuhakikisha inaichapa Real Madrid wakiwa kwenye uwanja wa wake wa nyumbani ili kujihakikishia kubaki katika mashindano hayo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Miamba hiyo ya Ujerumani haijapoteza mchezo hata mmoja nyumbani katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa msimu huu.

Madrid inashuka jijini Munich ikiwa na faida ya ushindi wa bao 1-0, shukrani kwa bao la dakika ya 19 la Karim Benzema kwenye mchezo wa
Jumatano iliyopita.

Bayern haijawahi kupoteza dhidi ya Real katika michezo yote iliyopigwa mjini Munich, wakiwa na  historia ya ushindi katika michezo minane na sare moja, ikifikisha idadi ya ushindi katika michezo 11 dhidi ya Madrid na jumla ya michezo yote kwa timu hizo kukutana ni 21.

Real wameendeleza kiwango chao kizuri tangu walipoifunga Barcelona katika fainali ya Kombe la Mfalme na kuichapa  Bayern kabla ya kuitandika Osasuna kwa mabao 4-0 juzi.

Mchezaji Bora wa Dunia, Cristiano Ronaldo alithibitisha kuwa yuko fiti kuivaa Bayern baada ya kuwa nje kutokana na maumivu ya misuli na alifanikiwa kufunga mara mbili na kumfanya afikishe mabao 47 aliyofunga msimu huu.

Kwa upande wa kocha Pep Guardiola, ameiongoza  Bayern vizuri na kukubali kuruhusu bao katika michezo yake tisa ya mwisho tangu walipotwaa ubingwa wa Bundesliga, wakiwa na rekodi ya ubingwa huo wa mapema wakiwa na mechi saba mkononi mwezi uliopita.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC