Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MBUYU TWITE AWEKA HADHARANI UCHAWI WA SIMBA

DUNIANI kuna mambo, kwani beki wa Yanga Mbuyu Twite amesema inawezekana mashabiki jukwaani waliokuwa wakifuatilia mechi yao dhidi ya Simba juzi Jumamosi waliona kila kitu kinaenda sawa kwao,lakini ukweli ni kwamba yeye na wachezaji wenzake walikuwa wanajiona wazito kiasi cha kucheza chini ya kiwango.

Mechi hiyo ya mwisho ya msimu wa Ligi Kuu Bara wa 2013/14 iliisha kwa sare ya bao 1-1, iliishuhudia Simba ikitawala sehemu ya kiungo kwa muda fulani kwa wachezaji wake Jonas Mkude na Said Ndemla kucheza wanavyotaka mbele ya Frank Domayo na Hassan Dilunga.

Lakini beki wa kulia wa Yanga, Twite alisema: “Tulikuwa hatujielewi uwanjani, ndiyo maana kuna wakati Simba walionekana kutawala sana kiungo maana ni kama tulifungwa mawe hivi, tulikuwa katika wakati mgumu tukiwa vyumbani wakati wa mapumziko baada ya kila mchezaji kulalamika kujiona mzito.

“Pumzi zilitubana muda wote hasa tuliokuwa tunakimbia sana uwanjani, nilishangaa sana kwani kabla ya kuja uwanjani hatukujisikia hivyo.”


Kuna taarifa zilizoeleza kuwa na hewa nzito katika chumba cha kubadilishia nguo cha wachezaji wa Yanga na alipotafutwa Daktari wa Yanga, Juma Sufiani alisema: “Kila mchezaji alikuwa akilalamika kuwa amekuwa mzito ghafla, hawakuwa hivyo kabla ya kufika uwanjani, siwezi kuthibitisha moja kwa moja kama kuna kitu kilipulizwa vyumbani au la. Tupe muda tufanye uchunguzi.”

Chanzo Mwanaspoti

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC