Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAOMBI YA ARSENE WENGER YAJIBIWA

Man City 2-2 Sunderland
Maombi ya kocha ,wa Arsenal Arsene Wenger ya kuitaka Everton ishindwe ilikuisaidia timu yake kufuzu kwa kombe la mabingwa msimu ujao yalitimia hapo jana ,Crystal Palace ilipoilaza Everton mabao 3-2 na
kuiruhusu Arsenal kusalia katika nafasi ya nne ikiwa na alama 67 alama moja zaidi ya Everton.


Wenger ambaye ameshuhudia timu yake ikidorora kutoka nafasi ya kwanza mwezi januari hadi ya tano mapema juma hili amesema hiyo ndiyo ombi lake kuu ya kuhakikisha Arsenal inamaliza katika nafasi ya nne bora na kufuzu
kwa ligi kuu ya mabingwa barani Ulaya msimu ujao.
Crystal Palace 3-2 Everton
Katika mechi nyingine iliyochezwa jana usiku ,azimio la Manchester City kutwaa kombe la ligi hiyo ya Uingereza yalipata pigo baada ya timu hiyo kutoka sare ya 2-2 dhidi ya Sunderland.
Bao la kwanza lilipachikwa wavuni na Fernandinho kunako dakika ya 2.
Man City 2-2 Sunderland

Ratiba ya Man City

  • Mon 21 April: v West Brom (H)
  • Sun 27 April: v Crystal Palace (A)
  • Sat 3 May: v Everton (A)
  • Wed 7 May: v Aston Villa (H)
  • Sun 11 May: v West Ham (H)
Sunderland ilisawazisha kunako dakika ya 73 na kuongeza lingine dakika kumi baadaye kupitia kwa mchezaji Wikham.
Nasri ndiye aliyemuokoa kocha Manuel Pelligrini aibu ya kushindwa alipofunga bao la kusawazisha kunako dakika ya 88 ya mechi hiyo.

Kutokana na matokeo hayo Pelligrini sasa anategemea matokeo ya vinara wa ligi hiyo Liverpool na Chelsea kubaini matumani yake ya kutwaa taji la mwaka huu.

The Reds ndio wanaoongoza jedwali la ligi na alama 77 ikifuatiwa na Chelsea ikiwa na alama 75.
Man city inashikilia nambari ya tatu kwa alama 71.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC