Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MANISPAA ILALA YAIPIGA MARUFUKU YANGA KUJENGA UWANJA JANGWANI

Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa amepigilia msumari wa mwisho kwa kuwataka Yanga kusahau kuhusu ongezeko la eneo la kujenga uwanja wake eneo la Jangwani kwa vile sehemu hiyo ni mkondo wa maji.

Akizungumza, Dar es Salaam jana, Silaa alisema:

“Tumepata hasara kubwa (Serikali) hii yote imetokana na watu kujimegea maeneo na kujenga kwenye mkondo wa maji, mafuriko yote haya yanayotokea ni kwa vile maji yanakosa pa kwenda na kuishia kwenye maeneo mengine ndiyo maafa yote haya yanatokea.


“Hebu angalieni pale Jangwani sasa hivi kulivyo, maji yamefurika watu wengine wamepoteza maisha, halafu bado turuhusu watu waendelee kujenga kwenye mkondo wa bahari, waambieni wasahau hilo.”

Kauli hiyo ya Meya Silaa imekuja siku chache baada ya Baraza la Mazingira la Taifa (NEMC) kudai kuwa eneo ambalo wanaliomba Yanga ni hatarishi, hivyo watafute eneo lingine kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wao kama kweli uongozi uliopo chini ya Mwenyekiti wake, Yusuf Manji, una nia ya kuwajengea Wanayanga uwanja.

Eneo hilo la Jangwani, mbali ya kuwa ni bonde kubwa la Mto Msimbazi, ambalo ni mkondo wa upumuaji wa bahari, lakini pia kuna bomba kubwa linalopeleka maji Hospitali ya Taifa Muhimbili na lingine linalopeleka maji taka baharini.

Hata hivyo, licha ya Yanga kushauri kuondoka eneo hilo ambalo ni hatarishi, uongozi wa klabu hiyo chini ya Mwenyekiti wake wa

Ujenzi wa Uwanja, Francis Kifukwe, umezidi kusisitiza kuwa kuna masharti ambayo NEMC wamewapa na wakiyatimiza eneo hilo watapewa ikiwemo kubeba fidia za kuwalipa wakazi wa eneo hilo.

“Kuna masharti ambayo wametupa na sisi tupo tayari kuyatekeleza hawajatuambia chochote, huyo aliyekwambia tumenyimwa kujenga uwanja ni nani? Nitajie huyo mtu wa NEMC, ninachoweza kusema kuna masharti na maelekezo ambayo wametupa,” alisema Kifukwe huku akigoma kuzungumzia suala hilo kwa undani kwa kueleza masharti na mapendekezo waliyopewa.

Kamati ya Mipango Miji na Mazingira ya Manispaa ya Ilala ilikutana hivi karibuni kujadili suala hilo ambalo hata hivyo wameliacha  mikononi mwa NEMC.

Nayo Kamati ya Mipango Miji na Mazingira ya Manispaa ya Ilala ilifanya  ziara ya ukaguzi wa Jangwani hivi karibuni

Wakati huohuo; Mvua hizo zinazoendelea kunyesha zimesababisha ukuta mkubwa wa uzio wa uwanja wa Yanga, ambao umejaa maji kwa sasa kubomoka. Ukuta huo ni ule ambao upo upande wa bonde la Msimbazi chini ya uwanja huo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...