Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAMBO UWANJANI YANG'ARA KIMATAIFA, DIAMOND, MOSES OLOYA WATIKISA

Na Elias John

MTANDAO wa Mambo Uwanjani unaomilikiwa na Prince Hoza ambao umefikisha mwaka mmoja tangia kuanzishwa kwake umeweza kung'ara hasa kutokana na idadi kubwa ya wasomaji wake ndani na nje ya Tanzania.

Hadi sasa mtandao huo umetazamwa na watu wasiopungua milioni moja huku nchi za Tanzania, Marekani, Uingereza na Uholanzi zikiongoza kwa kuwa na watazamaji wengi zaidi duniani.

Nchi ya Kenya inafuatia kwa ukanda wa Afrika mashariki wakati India inaongoza kwa upande wa bara Asia, takwimu hizo zilizotolewa kufuatana na mpangilio wa utazamwaji wa mtandao huo wa habari unaonyesha kuwa nchi za Ulaya na Amerika ndizo zenye watazamaji wengi zaidi.


Msanii Nasseb Abdul maarufu Diamond Platinum na mshambuliaji wa timu ya taifa ya Uganda Moses Oloya ndio vinara kwa kujizolea wasomaji lukuki ambao wamekuwa wakizisoma taarifa zao.

1-Diamond Platinum

Diamond anaongoza kwa kusomwa zaidi huku akifuatiwa na mchezaji Moses Oloya ambaye alijipatia wasomaji wengi wakati anataka kusajiliwa na vilabu vya Simba na Yanga.

2-Moses Oloya anakamata nafasi ya pili, habari zake za kuwaniwa na vilabu vya Simba na Yanga zilimwezesha kutazamwa na idadi kubwa ya watu na kumfanya ashike nafasi hiyo.

3-Meneja wa kundi la sanaa la Super shine Modern Taarab Kais musa Kais anakamata nafasi tatu, Kais ameingia katika kundi la watu maarufu wanaotazamwa sana kutokana na kufiwa na mke wake Nyawana Fundikira ambaye alikuwa mtangazaji na mwimbaji wa taarabu.

4-Vifo vya wanajeshi saba wa Tanzania huko Darfur Sudan vimeingia katika orodha ya taarifa gumzo zaidi katika mtandao huo, wanajeshi hao waliuawa katika mlipuko wa bomu uliofanywa na waasi huko Darfur.

5-Mlinda lango Juma Kaseja ambaye alitemwa na timu yake ya Simba naye alipata umaarufu na kuandikwa sana mitandaoni, Kaseja alikuwa akimulikwa na vilabu mbalimbali ambapo vilitaka kumsajili, timu ya Mtibwa Sugar ndio iliyotaka kumsajili ambapo taarifa zake ziliandikwa na mtandao huu na kutembelewa na watu wengi.

6-Mwanamuziki aliyejitangaza ni mfuasi wa Freemason mwenye maskani yake jijini Tanga Mkola Man aliingia katika nafasi hiyo huku habari zake zikitazamwa na watu wengi.

7-Tamasha la Simba Day ambalo huandaliwa na klabu ya Simba lilikamata nafasi ya saba huku wachezaji Mrisho Ngasa na Moses Oloya wakitangazwa kutambulishwa katika tamasha hilo, Oloya alikuwa akitakiwa na Yanga huku Ngasa tayari alishatangazwa na Yanga kama mchezaji mpya.

8-Sakata la mshambuliaji wa Liverpool ya England Luis Suarez nalo liliweza kukonga vichwa vya habari mbalimbali duniani, Suarez amekamata nafasi ya nane katika mtandao huo.

9-Mtangazaji wa kipindi cha michezo cha redio Clouds Shaffih Dauda naye amechomoza hadi nafasi ya tisa, kupingana kwake na TFF iliyokuwa chini yake Leodegar Tenga kulipelekea kushutumiwa vikali na ndipo habari zake zilipopata kutazamwa sana.

10-Mshambuliaji na mchezaji bora wa dunia Cristiano Ronaldo anayekipiga Real Madrid ya Hispania alitajwa mapema kama atachukua tuzo ya mchezaji bora wa dunia

.Ronaldo alikuwa akipewa nafasi kubwa kutokana na mchango wake mkubwa alioutoa katika klabu yake na timu ya taifa ya Ureno iliyofuzu kwa fainali za kombe la dunia zitakazofanyika nchini Brazil mwaka huu.

AZUNGUMZIA MAENDELEO YA BLOGU YAKE

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mkurugenzi wa Mambo Uwanjani Publishers ambao ndio wamiliki na watayarishaji wa blogu hiyo Prince Salum Hoza ambaye pia ni mwandishi wa habari amesema bado jitihada zinaendelea ili kufikia malengo.

'Malengo yangu kuifanya blogu hii iwe ya Watanzanjia wote bila kujali itikadi wala nini, hii ni blogu ya kijamii hakuna Usimba wala Uyanga pia itikadi za kisiasa tumeziweka kando', alisema na kuongeza

.'Masuala ya kupendelea CCM, Chadema au CUF hapa hilo hakuna isipokuwa tunajali uzalendo, pia hatuna ubaguzi wa kidini, rangi wala jinsia tunazipa umuhimu habari zote', aliongeza.

Kuhusu idadi ya waandishi wanaotumikia Mambo uwanjani blogspot, Hoza amedai mpaka sasa hakuna idadi kamili ya waandishi kwakuwa bado changamoto zinaendelea.'Kwa sasa nina waandishi wasiopungua wanne ambao ni Exipedito Mataruma, Elias John, Regina Mkonde, Salum Fikiri na mimi mwenyewe', aliongeza.

MATARAJIO YA BAADAYE

Hoza amesema malengo yake yatakamilika endapo blogu yake itapata matangazo ya kutosha, anamshukuru mdhamini wake Chifu Panduka na Angaza House Agent ambao wamekuwa wakimwezesha mara kwa mara, pia anawashukuru wadau wote ambao wamekuwa watazamaji wazuri na kumpa nguvu.

Kuhusu maendeleo mengine amesema mpaka sasa kampuni yake inamiliki blogu mbili ambazo ni Mambo uwanjani blogspot na Staa wa leo, aidha Hoza ameongeza kuwa ana mipango ya kuanzisha gazeti lake la michezo kwa lengo la kuzipa sapoti blogu zake

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC