Ruka hadi kwenye maudhui makuu

LOGARUSIC AWAAHIDI USHINDI SIMBA KESHO

Kocha wa Simba, Zdavko Logarusic, amewatoa shaka mashabiki wa timu hiyo waliopoteza furaha kwa kuwaambia kuwa kipigo alichoipa Yanga katika pambano la Nani Mtani Jembe atakiendeleza kesho.

Simba na Yanga zitashuka uwanjani kesho kukabiliana katika moja ya mapambano ya hitimisho la Ligi Kuu Tanzania Bara litakalopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Simba, wameambulia patupu msimu huu baada ya Azam FC kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwake, huku wapinzani wao, Yanga wakivuna nafasi ya pili.


Katika pambano la Nani Mtani Jembe lililopigwa Desemba 21 mwaka jana kwenye Uwanja wa Taifa, Simba iliichakaza Yanga kwa mabao 3-1.

Akizungumza na gazeti hili kwa simu kutoka Zanzibar jana, Logarusic, alisema: “Nafahamu wapo mashabiki wetu ambao wamekata tamaa baada ya timu yao kuukosa ubingwa na hakika ni kitu kilichonisikitisha hata mimi, lakini niseme kwamba tutafurahi pamoja Jumamosi.

“Hawana sababu ya kuwa na presha kwa vile Yanga tuliyocheza nayo Desemba ndiyo hiyo hiyo tutakayocheza nayo Jumamosi sijaona kama imebadilika  kiasi ambacho iwe tishio kwa timu yangu.

“Nimewaambia wachezaji wangu huu ndiyo mchezo ambao tunatakiwa kuutumia kurudisha imani kwa mashabiki wetu, duniani kote ukiondoa ubingwa ambao kila mmoja anauhitaji, jambo jingine la maana ni kumfunga mpinzani wako, kitu ambacho sioni sababu ya sisi kushindwa.”

Alisema hahofii lolote hata kama kuna maneno kuwa atafukuzwa kwani kocha yeyote inabidi awe tayari kwa lolote, lakini amewaomba wachezaji wake waifunge Yanga kesho ili wasiaibike.

Kocha huyo mwenye vituko vingi awapo uwanjani anaamini timu yake itaibuka na ushindi mbele ya Yanga na kudai ukubwa wa majina ya wapinzani wao wala haumtishi kwani wanaingia uwanjani kusaka heshima, hivyo wachezaji wake hawapaswi kuwa na presha ya mchezo.

“Tumekosa vyote na tutaendelea kuwa watazamaji kwenye michuano ya kimataifa, tangu mwanzo tulipotea, hatukujipanga, lakini hatupaswi kuangalia hayo na sasa tunacheza mechi ya mwisho ili kusaka heshima tu.

“Wachezaji wanapaswa kujua hilo, ushindi katika mechi hii ni lazima na wala wasiwe na presha kwani mchezo huu ni wa kawaida, hivyo tutaingia tukiwa hatuna presha zaidi ya kutaka ushindi na kutunza heshima yetu kwani haitapendeza kama tutapoteza mchezo huu, tutaaibika, tukose hata nafasi ya nne?!

“Yanga ni timu kubwa na nzuri na imefanya vizuri msimu huu licha ya kukosa ubingwa, lakini hatupaswi kuogopa ukubwa wa majina ya wachezaji wao, tuko tayari kukabiliana nao,” aliongeza kocha huyo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC