Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BUNGE LA KATIBA KUVUNJIKA

Hatua ya baadhi ya wajumbe wa Bunge la Katiba kususia vikao vya Bunge hilo imezua hofu kwamba inaweza kukwamisha mchakato wa kupatikana kwa Katiba mpya hasa katika kufanya uamuzi wa kupitisha ibara za Katiba hiyo.

Wajumbe ambao ni wanachama wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), juzi walitoka nje na kususia vikao vya Bunge hilo kwa madai kwamba hawaridhishwi jinsi mambo yanavyokwenda.

Kanuni za uendeshaji wa Bunge hilo za 2014, zinasema ili ibara au Rasimu ya Katiba iweze kupitishwa itahitaji kuungwa mkono na theluthi mbili ya wajumbe kwa pande zote za Muungano.


Kanuni ya 37 (1), inasomeka: “… ili ibara au rasimu iweze kupitishwa, itahitaji kuungwa mkono na wingi wa theluthi mbili ya wajumbe kutoka Tanzania Bara na theluthi mbili kutoka Zanzibar.”

Taarifa zisizo rasmi zinasema awali ili kuwezesha kupatikana kwa theluthi mbili kutoka upande wa Zanzibar, CCM kilikuwa kinakihitaji kupata kura 16 ikilinganishwa na idadi ya wajumbe wanaokiunga mkono.

Kwa maana hiyo kuondoka kwa wanachama wa Ukawa kunamaanisha kwamba Bunge Maalumu haliwezi kupata akidi inayotakiwa wakati wa kufanya uamuzi wa kupitisha ibara kwa mujibu wa kanuni hizo.

Mwenyekiti mwenza wa Ukawa, Profesa Ibrahim Lipumba alisema jana kuwa hawatarejea katika Bunge hilo hadi kutakapokuwa na maridhiano ambayo kwa upande wao ni kuzingatiwa kwa rasimu iliyotokana na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba. Katibu wa Bunge Maalumu, Yahya Khamis Hamad alisema hivi sasa si vyema kutabiri kama wajumbe wa Ukawa watarejea bungeni au la.

“Mimi na wewe hatuwezi kutabiri, maana hawa ni viongozi wa kisiasa, wanaweza kuondoka leo, lakini kesho wakawa na mazungumzo na wenzao halafu wakarejea bungeni na shughuli zikaendelea,” alisema Hamad na kuongeza:

“Ni kweli kwamba kutokuwapo kwao kunaweza kuwa na athari katika kufanya uamuzi, lakini pia hatuwezi kusema ni athari zipi kwa sasa kwa sababu hakuna suala ambalo linapaswa kufanyiwa uamuzi kwa sasa.”

Hamad alisema kama alivyosema Mwenyekiti wa Bunge Maalumu, Samuel Sitta ipo fursa za kufanya mazungumzo na kwamba anaamini ikitumika vizuri, Bunge litaweza kuendelea na kufikia mwisho mwema.

“Kwa hiyo mimi nasema sisi tusubiri, maana hadi sasa hatujapata kufahamu kama kuondoka kwao watarejea baada ya Pasaka, Jumanne ijayo au ndiyo wameondoka moja kwa moja au ni vipi, ndiyo maana nasema ni vigumu kudhania kitakachotokea,” alisema Hamad ambaye pia ni Katibu wa Baraza la Wawakilishi.

Wasusia Kamati ya Uongozi

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC