Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AZAM FC YAVURUGA MAPATO YA SIMBA NA YANGA

Kuibukia kwa mafanikio kwa timu ya Azam FC na kufanya vibaya kwa miamba ya soka nchini kumeanza kuzipa machungu ya kiuchumi timu za Simba na Yanga, ambazo katika mechi iliyopita baina ya watani hao wa jadi ziliingiza mapato kiduchu ya Sh. milioni 130, ambayo ni madogo zaidi kupatikana katika miaka ya karibuni tangu ulipojengwa uwanja mpya wa Taifa 2007.

Katika taarifa ya uongozi wa Simba iliyotolewa mwanzoni mwa wiki kuhusu tathimini yao kwa msimu huu, katibu mkuu wa klabu hiyo ya Msimbazi, Ezekiel Kamwaga alisema walikuwa wakiambulia mgawo wa mapato wa hadi Sh.300,000 katika baadhi ya mechi zao ikiwamo dhidi ya Ashanti United ambayo walilala 1-0.


Mechi baina ya Simba na Yanga ambayo kwa kawaida huwa na mashamsham tele nchi nzima, ya kufungia msimu huu ya Aprili 19, 2014 iligeuka kuwa kama mechi ya "ndondo" ikichezwa huku Azam ikiwa tayari imeshatwaa ubingwa wa bara kwa mara ya kwanza tangu ilipopanda daraja 2008.

Mashabiki wachache mno walihudhuria kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam katika mechi hiyo iliyokosa mvuto huku shamrashamra zikitawala "upande wa pili" kwenye uwanja wa Azam Complex ambako Azam walikuwa wakikabidhiwa kombe lao na kuwashuhudia mashabiki wote walioingia siku hiyo wakipewa chakula na vinywaji bure.

Mapato ya Sh. milioni 130 yaliyozishuhudia timu hizo kila moja ikiambulia mgawo wa Sh. milioni 30, yalikuwa ni pigo kiuchumi kwa timu hizo zinazotegemea kwa kiasi kikubwa mapato makubwa ya mechi baina yao kwa ajili ya "kuzibia mashimo" mengi katika kujiendesha kila msimu.

Kufikia sasa, rekodi ya mapato ya mechi baina ya Simba na Yanga ni ya raundi ya kwanza msimu huu iliyomalizika kwa sare ya 3-3 ambayo iliingiza Sh. milioni 500.7.

Rekodi ya awali ya mapato ya mechi baina ya miamba hao wawili wa soka nchini ilikuwa ni Sh. milioni 500.4, iliyopatikana katika mechi ya kufungia msimu uliopita ambayo Yanga ilishinda 2-0 Mei 18, 2013.

Kushuka kwa mapato katika mechi za Simba na zile za Yanga msimu huu kumechangiwa na kiwango kisichoridhishwa cha timu hizo zinazopendwa na mashabiki wengi zaidi nchini ambazo zitalazimika kujipanga zaidi msimu ujao ili kuwarejesha mashabiki wao viwanjani.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC