Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AZAM FC YAHAMISHIA MAKALI YAKE KLABU BINGWA AFRIKA

Baada ya kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2013/14, benchi la Azam FC limewapa likizo ya wiki saba wachezaji wake ili wapumzike kabla ya kuanza maandalizi ya msimu mpya wa ligi hiyo 2014/15 na mashindano ya kimataifa.

Azam FC imetwaa ubingwa wa ligi hiyo kwa mara ya kwanza tangu ipande Ligi Kuu 2007 baada ya kumaliza kileleni ikiwa na pointi 62 ilizozipata bila kupoteza hata mechi moja kati ya mechi 26 zote za ligi.


Akizungumza katika mahojiano maalum mara tu baada ya kumalizika kwa mechi yao ya mwisho waliyoshinda 1-0 dhidi ya JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Azam jijini Dar es Salaam juzi, Joseph Omog, kocha wa Azam FC, alisema nyota wake watapumzika kwa muda huo kabla ya kuingia kambini kujiweka sawa kwa ajili ya msimu ujao na mashindano ya kimataifa.

"Wachezaji wetu wamefanya kazi kubwa na wamechoka sana, itabidi wapumzike kwa wiki saba ili wapate nguvu ya kuanza maandalizi ya msimu ujao," alisema Omog.

"Tukisharejea, tutaingia kambini molja kwa moja tukianza na kambi ya ndani ya Tanzania lakini baadaye tutapiga kambi nje ya mipaka ya nchi hii ili tucheze mechi nyingi zaidi za kirafiki kabla ya kushiriki michuano ya Klabu Bingwa Afrika Februari mwakani," alisema zaidi raia huyo wa Cameroon.

Aidha, kocha huyo aliyewahi kutwaa taji la Kombe la Shirikisho barani Afrika akikinoa kikosi cxha Leopards ya Congo, alisema mwishoni mwa wiki hii atakwenda kwao Cameroon kwa mapumziko kabla ya kuanza maandalizi ya msimu mpya.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC