Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ANELKA KUTOCHEZA BRAZIL

Nicholas Anelka

Klabu cha Brazil Atletico Mineiro kimetangaza wamefutilia mbali mipango ya kumsaini straika wa Ufaransa, Nicolas Anelka.

Mkurugenzi wa timu hiyo Eduardo Maluf amesema kuwa Mineiro wameshindwa katika juhudi zao za kuwasiliana na mshambuliaji huyo aliyechezea Arsenal, Real Madrid, Paris Saint Germain na Chelsea na wamekata tama ya kusajili nyota huyo aliye na umri wa 35.

“Hakuna wakati tulifanikiwa kuzungumza naye,” vyombo vya habari vya Brazil vilinukuu Maluf akisema.

Miniero walidhibitishia AFP kuwa Anelka hatajiunga na gwiji wa Brazil, Ronaldinho, anayesakata kabumbu yake kwenye timu hiyo huku Maluf akiongeza watatuma malalamishi kwa shirkisho la soka duniani, FIFA, kuhusu straika huyo.


Mkurugenzi huyo anashikilia kuwa waliaafikiana na waakilishi wa Anelka lakini wakala wake, Cristian Cazini, aliwapasha habari kuwa mchezaji huyo hatawasili Brazil Jumamosi iliyopita kama ilivyopangiwa.
“Tuliamua kandarasi hiyo imebatilishwa kwani hatutasubiri hadi tarehe 19,” Maluf alifafanua.

Mwenyekiti wa Mineiro Alexandre Kalil alisema Aprili 5 kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter kuwa Anelka atasaini huku wanahabari wa Brazil wakichapisha picha za mashabiki wa klabu hicho wakibeba mabango ya kumkaribisha straika huyo.

Anelka alisafiri Kuwait kuhudhuria kongamano la vijana wa dini ya Kiislamu badala ya kutua Brazil kukamilisha maagano kati yake na Miniero.

Maluf alifichua kuwa mkataba ulikuwa mezani ukingoja sahihi yake uliaafikia angelicheza nao hadi Desemba mwaka ujao.

Klabu cha Ligi ya Premier ya Uingereza, West Bromwich Albion kilimfuta Anelka mwezi uliopita kwa upotuvu wa nidhamu baada ya kuonekana kuonyesha ishara ya kupinga usemiti ‘quenelle’ baada ya kuwafungia bao.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC