Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AMISSI TAMBWE KUTIMKA RASMI SIMBA LEO

Mshambuliaji Amisi Tambwe wa Simba anatarajia kuondoka nchini leo kurejea kwao Burundi kwa ajili ya mapumziko huku akiweka wazi kwamba akifika nyumbani atapata jibu la kujiunga na Yanga, Azam FC au kutimkia Uarabuni huku akiweka wazi nia yake ya kutaka kucheza Ligi ya Klabu Bingwa Afrika ama Kombe la Shirikisho.

Akizungumza katika mahojiano maalum jijini Dar es Salaam jana mchana, Tambwe ambaye ni mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2013/14, alisema akiwa nyumbani kwake Burundi, atakuwa na muda mzuri wa kufikiri na kuchagua timu sahihi ya kuichezea msimu ujao.


"Bado mimi nina mali ya Simba lakini klabu inatambua pia kwamba ninahitaji kupata maslahi mazuri zaidi. Nimefuatwa na watu waliodai wametumwa na klabu za Yanga na Azam lakini mpaka sasa sijapata jibu la timu ipi niikubalie ofa yake," alisema.

"Kesho (leo) mimi na Kaze (Gilbert) tunatarajia kusafiri kurejea nyumbani kupumzika. Nikishafika nyumbani nitazungumza kuhusu klabu ipi nitajiunga nayo msimu ujao.

Tofuati na Azam na Yanga, pia nimepata ofa ya timu kutoka Saud Arabia," alisema zaidi nyota huyo aliyeifungia Simba magoli 19 katika mechi 23 msimu huu.

Mwishoni mwa wiki, mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Burundi na Kombe la Kagame mwaka jana, Tambwe aliweka wazi nia yake ya kuondoka Simba, na amesema anatamani kucheza katika Ligi ya Klabu Bingwa Afrika au Kombe la Shirikisho, kauli ambayo inaonyesha kuvutiwa kwake na kujiunga na Azam ama Yanga ambazo zitaiwakilisha nchi katika michuano hiyo msimu ujao.

Klabu yake ya Simba imekosa tena nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa baada ya kumaliza katika nafasi ya nne ya msimimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Tayari uongozi wa 'Wekundu wa Msimbazi' kupitia kwa mwenyekiti wa kamati ya usajili, Zacharia Hanspope umeshasema hautamzuia mkali huyo wa mabao kuvunja mkataba wake na klabu hiyo uliobakisha mwaka mmoja endapo akipata timu itakayompa maslahi mazuri zaidi.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC