Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AMISSI TAMBWE AKANUSHA KUIHAMA SIMBA

Na Regina Mkonde.

Straika wa timu ya wekundu wa msimbazi Simba Amissi Tambwe amekanusha taarifa ambazo zilikuwa zinavumishwa na baadhi ya vyombo vya habari kwamba amefanya mazungumzo na baadhi ya timu hapa nchini ili ahame Simba.

Maneno hayo aliyazungumza Amissi Tambwe akiwa katika kiwanja cha mazoezi cha Kinesi wakijiandaa na mechi  ya watani wao wa jadi Yanga ambayo itachezwa jumamosi ijayo.

'Mimi sijawahi kuongea na vyombo vya habari juu ya suala hili na hata uongozi wa timu yoyote ile ila ninacho shangaa kusikia kwenye vyombo vya habari kwamba Tambwe anataka kuhama Simba', Alisema na kuongeza straika huyo.


'Mpaka sasa sijapata taarifa yoyote kutoka kwa viongozi wangu ya mimi kuhama isitoshe mkataba wangu bado haujaisha nimesajiliwa Simba mwaka jana mkataba wa miaka miwili inamaana mkataba wangu unaisha mwaka 2015 iweje leo vyombo vya habari vinanivumisha nataka kuhama Simba Sc?', alishangaa mchezaji huyo anayetokea nchi ya Burundi Amissi Tambwe.

'Kuhusu taratibu zetu za kisoka mtu ambaye mkataba wake haujaisha haruhusiwi kusaini mkataba wa timu nyingine labda viongozi wenyewe waamue kuniuza hapo sitakataa ila ninaamini viongozi wangu na wadau wa timu ya Simba Sc hawawezi wakaniuza kwa sasa',aliongeza Tambwe.

Tambwe mpaka sasa ameshikilia rekodi ya mfungaji bora katika msimu huu wa ligi kuu Tanzania bara inayodhaminiwa na Vodacom Tambwe amefunga magoli 19,  alieleza changamoto alizokutana nazo katika msimu huu na kudai kuwa alisaini mkataba wa Simba ili ahakikishe timu yake inachukua ubingwa lakini hicho kitendo kimekuwa kinyume na kuacha mchezaji huyo abaki njia panda.

Nilijitahidi kweli kufunga katika msimu huu ila ndiyo hivyo timu yangu haijafanikiwa kupata nafasi ya kuchukua ubingwa ingawa baadhi ya watu wanamlaumu kocha Zdravoc Logarusic na kudai kuwa si kocha mzuri mimi siafikiani nao sababu ni kocha anayefaa kupormoka kwa timu ni bahati mbaya tu.Alisema Amis Tambwe.

Tambwe ambaye hapo awali alishawahi kucheza timu kama MountozFc  Black Eagle na Vitalo Fc za nchini kwao Burundi alikuwa akisifika kwa uwezo wake akiwa mpirani na timu zote alizopita Tambwe alikuwa akiongoza kwa kufunga mabao.

Siku chache zilizopita Tambwe alipigwa faini na shirikisho la mpira wa miguu TFF kwa kosa la kutukana akiwa uwanjani tukio hilo lilitokea wakati Simba Sc ilipocheza na Mbeya City Amissi Tambwe baada ya kufunga goli alinyoosha kidole cha shahada ila TFF ilimnukuu vibaya na kumwambia alionyesha kidole cha kati ambacho kinamaanisha tusi.

Tambwe alisikitishwa na kitendo hicho sababu alilipishwa faini ya sh laki tano za kitanzania na kosa hili si sahihi sababu hakuna uthibitisho wa video ulionyesha mchezaji huyo akionyesha ishara ya kunyoosha kidole cha kati ambacho kinatafsiri ni matusi.

Mpaka sasa Tambwe amebakisha mkataba wa mwaka mmoja naye amesema kuwa mechi waliyoibakiza ni ya ushindani mkubwa sababu Simba itacheza na watani wao wa jadi.mechi hii inatakiwa tufunge ili kuleta heshima ya timu ila sitaongea mengi kwa kuwa mchezo hautabiliki ila tunachotakiwa ni kushinda', Alisema Tambwe.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC