Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AIBU MABONDIA WA TANZANIA, WOTE WANUSURIKA KUUAWA

BONDIA Francis Miyeyusho amepigwa na mpinzani wake, Sukkassem Kietyongyuth wa Thailand kwa Knockout (KO) raundi ya kwanza sekunde ya 55 katika pambano la raundi 10 lisilo la ubingwa, uzito wa Feather lililofanyika ukumbi wa PTA, Temeke, Dar es Salaam usiku wa jumamosi.

Katika pambano hilo lililohudhuriwa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Suleiman Kova aliyekuwa mgeni rasmi, Miyeyusho aligoma kupanda ulingoni kwa dakika zaidi ya 20 akishinikiza kwanza alipwe fedha zake.

Kamanda Kova ambaye mdogo wake, Mussa Kova ndiye aliyeandaa mapambano hayo kupitia kampuni yake ya Mawenzi Production, aliingilia sakata hilo na bondia huyo akalipwa fedha zake akapanda ulingoni.


Dalili za Miyeyusho ‘Chichi Mawe’ kupigwa zilionekana wakati nyimbo za taifa zinapigwa, kwani alikuwa asiyejiamini na mwenye kihoro, hivyo kumpa nafasi Mthailand kulianza kwa kasi pambano hilo.

Mgeni alianza kumtandika Miyeyusho tangu sekunde ya kwanza na ndani ya sekunde 20 bondia wa nyumbani alikaa chini akawahi kusimama, hata hivyo pigo hilo lilimuondoa mchezoni kabisa Chichi.

Mthailand aliibaini hali hiyo na akamfuata kwenye kamba Miyeyusho kumsukumia makonde mfululizo hadi refa Emmanuel Mlundwa alipokwenda kusimamisha pambano.

Refa alimpa nafasi Miyeyusho kuamua kuendelea au la na bondia huyo akajaribu kusogea mbele kurudi mchezoni, lakini akadondoka na Mlundwa akamaliza pambano, huku Chichi akisaidiwa na wasaidizi wake kuinuliwa chini kutolewa ulingoni.
 
Awali, Francis Cheka ‘SMG’ alitoshana nguvu na Gavad Zohrehvand wa Iran katika pambano lingine lisilo la ubingwa uzito wa Light Heavy raundi nane.

Hata hivyo, mashabiki walizomea matokeo ya sare katika pambano hilo, wakiamini Cheka alipoteza- kwani wazi mpinzani alionekana kutupa ngumi nyingi na raundi ya mwisho bondia wa Tanzania aliokolewa na kengele.

Ilionekana Cheka hakuwa na maandalizi mazuri kabla ya pambano lake la leo, kwani alikuwa ni mzito kutupa ngumi hadi kutembea ulingoni na alionekana kuanza kuchoka tangu raundi ya sita.

Katika mapambano ya utangulizi, Tasha Mjuaji alimshinda kwa pointi Steven Anastazi uzito wa Feather, Fabian Lyimo alimshinda Ramadhani Mnandi kwa pointi uzito wa Welter, Adam Yahya alimshinda kwa pointi Ramadhani Rajab uzito wa Light Fly na Sadik Momba alimshinda Epson John kwa pointi uzito wa Light, mapambano yote hayo raundi nne kila moja.
Ibrahim Class ‘Mawe’ alimshinda Mustafa Dotto kwa pointi pambano la raundi sita lisilo la ubingwa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC