Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA KUTIBUA NDOTO ZA AZAM KUTWAA UBINGWA WA BARA JUMAMOSI

Majaliwa ya Yanga na Azam FC kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara yapo mikononi mwa Simba ambayo imebakiza mechi na vigogo hivyo vinavyofukuzana kwa karibu katika msimamo wa ligi hiyo inayotarajiwa kumalizika Aprili 19, mwaka huu.

Azam ambayo ipo kileleni ikiwa na pointi 47, nne zaidi ya Yanga inayoshika nafasi ya pili, imebakiza mechi nne huku wapinzani wao wakibakiza tano, lakini zote zitalazimika kukutana na Simba, hivyo kupoteza dhidi ya Kikosi hicho cha Zdravko Logarusic kwa timu hizo kunaweza kupeperusha ndoto za kutwaa ubingwa.

Hata hivyo, Azam italazimika kuanza kushinda Jumamosi dhidi ya Simba kabla ya kujipanga kuibuka na ushindi itakapokutana na Ruvu Shooting ugenini na baadaye kuikabili Mbeya City kabla ya kumaliza na JKT Ruvu.


Wakati Yanga yenyewe itakuwa na kibarua kigumu dhidi ya  Tanzania Prisons kesho Taifa na Jumamosi kuifuata Mgambo JKT Uwanja wa Mkwakwani na baadaye kurudi Taifa kuialika JKT Ruvu.

Baada ya mechi hiyo, itasafiri kuifuata Oljoro JKT katika Uwanja wa Sheikh Kaluta Amri Abeid na kisha kumaliza na Simba Taifa.

Hata hivyo, kikwazo kingine cha Azam kinaweza kuwa Mbeya City ambayo ina kumbukumbu ya kupoteza mechi moja tu katika Uwanja wao wa Sokoine.

Tayari mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, Yanga, jana jioni waliingia kambini katika jengo la makao makuu ya klabu hiyo yaliyopo mtaa wa Jangwani na Mafia kwa ajili ya kujiandaa na mechi yao ya kesho dhidi ya Prisons kutoka jijini Mbeya.

Yanga imeamua kurejea kwenye makao makuu badala ya Bagamoyo kama ilivyotangaza kuwa ndiyo kambi yao ya kudumu msimu huu.

Kocha Msaidizi wa Yanga, Boniface Mkwasa, alisema kikosi hicho sasa hakitakuwa na mapumziko kwa sababu mechi zote zilizobakia ni ngumu na wao wanahitaji ushindi.Mkwasa alisema katika mbio za ubingwa hawapo peke yao, hivyo hawatakiwi 'kushangaa'.

"Hakuna kulala, tunajua kwamba sio peke yetu tunaotaka kikombe cha ubingwa, tunaendelea na mazoezi hakuna kupumzika," alisema kocha huyo wa zamani wa Ruvu Shooting.

Alisema kwamba Yanga imejiandaa kukutana na changamoto mbalimbali na ushindani kutoka kwa timu pinzani.
Aliongeza kuwa ligi ni ngumu na kila mchezaji anapaswa kujituma ili waweze kufikia malengo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC