Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SCHOLES ATAKA MOYES APEWE MUDA MAN UNITED

David Moyes

Kiungo wa kati wa zamani wa Manchester United Paul Scholes ametoa wito kwa mabingwa wa Uingereza ambao wamekuwa wakihangaika wasimteme meneja David Moyes licha ya kichapo kingine cha aibu.

Wiki moja tu baada ya kushindwa 3-0 nyumbani na mahasimu wao wa jadi Liverpool, United walilazwa kwa maabo sawa debi ya Manchester nyumbani kwao Old Trafford Jumanne.

Edin Dzeko alifungia Manchester City la kwanza sekunde ya 43 na straika huyo wa Bosnian akaongeza jingine mapema kipindi cha pili kabla ya Yaya Toure kukamilisha kichapo hicho kwa bao la tatu dakika ya 90.

Kichapo hicho kiliacha United wakiwa nambari saba ligini na alama 12 nyuma ya Arsenal walio nambari nne.
Hayo yameacha mashabiki wakiwa na mshangao, kwamba kikosi kile kile kilichoshinda ligi msimu uliopita na meneja wa zamani Alex Ferguson kabla ya kustaafu, kimekuwa hakijiwezi hivyo dhidi ya timu za Uingereza kikiwa mikononi mwa raia huyo wa Scotland ambaye alichaguliwa na Fergie.


Lakini Scholes alisema kumlaumu meneja huyo wa zamani wa Everton litakuwa kosa, akisema United wanafaa kumuunga mkono meneja huyo zaidi soko litakapofunguliwa kuliko walivyofanya kipindi kifupi ambacho Moyes amekuwa Old Trafford.

"Lazima msimame naye. Alinunua wachezaji kadha ambao hawajafana lakini majira ya joto atahitaji usaidizi zaidi, hakuna shaka kuhusu hilo,” Scholes aliambia Sky Sports Jumanne.
"Je aliungwa mkono ilivyotakikana majira ya joto yaliyopita? Sina uhakika kuhusu hilo, lakini majira yajayo lazima aungwe mkono na nafikiri kwamba anajua anahitaji wachezaji,” akaongeza mchezaji huyo wa zamani wa kimataifa wa Uingereza.

Nemanja Vidic anatarajiwa kuwaacha na kujiunga na Inter Milan mwisho wa msimu huku Rio Ferdinand na Patrice Evra wakiwa kwenye darubini.
Scholes alisema lazima Moyes aangazie kuimarisha safu ya ulinzi ya United, ingawa pia kumekuwepo wasiwasi kuhusu safu ya kati.

“Kwangu, inaonekana kuna ameneo kadha ambayo yanahitaji kuangazia,” Scholes, ambaye hatimaye alistaafu msimu uliopita, alisema.
"Sehemu ya kati ya safu ya kati unaweza kusema wamekuwa wakiangazia hilo kwa miaka kadha sasa na labda hawajapata jawabu mwafaka.

“Ninadhani ulinzi pia, ukizingatia kwamba Vidic anaenda – ni kama Rio na Evra pia wataenda, mabeki watatu kati ya wanne wako wanaenda – hiyo ni sehemu jingine ambayo anafaa kuangalia.
"Kwenda mbele, wako sawa. Lakini labda ni safu ya kati na ulinzi ambapo (Moyes) anafaa kuangazia.”

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC