Ruka hadi kwenye maudhui makuu

REAL MADRID YAKALISHWA NA BARCELONA 4-3, MESSI ADHIHIRISHA UCHAWI WAKE

MSHAMBULIAJI Lionel Messi amepiga hat-trick usiku wa jana Barcelona ikishinda 4-3 dhidi ya Real Madrid katika mchezo wa La Liga uliofanyika Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid.

Andres Iniesta alianza kuifungia Barcelona dakika ya saba, Karim Benzema akaisawazishia Real dakika ya 20 na kufunga la pili dakika ya 24.

Barcelona ikazinduka na kupata bao la kusawazisha dakika ya 42 kupitia kwa Messi, lakini Mwanasoka Bora wa Dunia, Cristiano Ronaldo akaifungia Real bao la tatu dakika ya 55 kwa penalti.

Messi akafunga mara mbili mfululizo kwa penalti dakika za 65 na 84 kukamilisha hat trick yake Barcelona ikifufua matumaini ya kutetea ubingwa wake msimu huu.


Real Ilimpoteza beki wake Sergio Ramos aliyetolewa nje kwa kadi nyekundu dakika ya 63 kwa kumuangusha Neymar kwenye eneo la hatari, wakati Pepe, Di Maria, Alonso, Modric na Ronaldo wote walionyeshwa kadi za njano na kwa upande wa Barcelona, Fabregas na Busquets pia walionywa kwa kadi za njano.

Kwa matokeo hayo Real inabaki na pointi zake 70, ingawa inaendelea kuongoza La Liga kwa wastani wa mabao, ikiwa inalingana pointi na Atletico Madrid, ambayo mapema iliifunga Real Betis 2-0, mabao ya Gabi dakika ya 58 na Diego Costa 64, wakati Barcelona inabaki nafasi ya tatu licha ya kufikisha pointi 69. Barca na Real zimecheza mechi 28 kila moja, wakati Atletico imecheza mechi moja zaidi.
  
Kikosi cha Real Madrid kilikuwa: Diego Lopez, Pepe, Ramos, Cristiano Ronaldo, Benzema/Varane dk64, Bale, Marcelo, Xabi Alonso, Carvajal, Modric/Morata dk90 na Di Maria/Isco dk85.

Barcelona: Valdes, Alves, Piqué, Mascherano, Jordi Alba, Sergio, Xavi, Iniesta, Fabregas/Sanchez, dk78, Messi na Neymar/Pedro dk69.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC