Ruka hadi kwenye maudhui makuu

RAGE AWAITA SIMBA MAMBUMBUMBU, ATANGAZA KUTOGOMBEA RASMI UENYEKITI

Wakati wanachama wa Simba wakipitisha mapendekezo ya marekebisho ya katiba yao, Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ismail Aden Rage ametangaza kutogombea tena nafasi hiyo jana asubuhi kwenye ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oysterbay.

Akizungumza kwenye mkutano huo wa marekebisho ya Katiba ya Simba, Rage alisema: “Simba oyee...Wanasimba msifanye makosa Mei 4 hakikisheni mnachagua kiongozi ambaye atakaa madarakani miaka minne, msifanye makosa baada ya mwaka mmoja mkataka aondoke, Katiba ya Simba inakataza mapinduzi.

“Mimi sitagombea, mimi siyo maskini, sina njaa, hata mkizomea nasemaje mimi sina njaa, na wanachama wengi mliopo hapa ni mambumbumbu.”

Kauli hiyo iliamsha hasira kwa baadhi ya wanachama ambao walitaka kumvamia na kumtwanga makonde, lakini Polisi waliingilia kati na kusababisha wanachama kupambana na wale wanaomuunga mkono Rage, tafrani hiyo ilidumu kwa zaidi ya nusu saa hadi pale Rage alipoomba radhi kwa kutangaza kuifuta kauli yake hali ikatulia na mkutano ukaanza.


Hata hivyo mkutano huo ulifanyika huku akidi ya wanachama ikiwa haijatimia kwani ili akidi itimie ilitakiwa kuwe na wanachama 250 na kuendelea, lakini wanachama waliofika jana ni 166 ambao hawafikii hata nusu ya akidi ya wanachama ambayo inatambulika kwa mujibu wa Katiba ya Simba.

Katika mkutano huo wanachama walipinga kuburuzwa kwa kuwepo kipengele cha ibara ya 11 (a) ambacho kinakataza mwanachama kuzungumza na vyombo vya habari isipokuwa vikao halali, na mwanachama atakayefanya hivyo tawi limuwajibishe ndani ya siku 14 tangu kutokea kwa kitendo hicho, wanachama hao waligoma na kutaka kifungu hicho kiondolewe kwani kinawaminya uhuru na haki ya kuzungumza.

Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, Geofrey Nyange naye alijikuta akizodolewa na Rage pale aliponyoosha kidole na kusema: “Taarifa mwenyekiti...taarifa, huku akisimama na kujibiwa na Rage ‘Siyo lazima usimame, kaa chini, nimesema siyo lazima, mwingine’ alisema Rage na kuteua mwanachama mwingine kuchangia hoja yake kabla ya kumpa nafasi Kaburu.

Akichangia kuhusu kipengele hicho Kaburu alisema: “Hakuna eneo ambalo TFF ilisema kuhusu kifungu hiki, haya ni mawazo yetu ni kweli baadhi ya wanachama wanatukana viongozi ndio maana kikawekwa ili kuminya wanachama wakorofi, kwa vile tupo hapa kwa ajili ya kuunda Kamati ya Maadili wakorofi wote watapelekwa kamati ya maadili ndio watawajibishwa huko siyo kuingiza kwenye katiba,” alisema Kaburu na kushangiliwa na wanachama wengi.

Kipengele kingine ambacho kinasubiri huruma ya TFF ambacho Simba wamekipitisha kwa kishindo ni kile cha ibara ya 26 kinachozungumzia sifa za wagombea, fasili ya tano ya katiba ya Simba ya zamani inasomeka: ‘Asiwe aliyewahi kutiwa hatiani kwa kosa la jinai kwa kuhukumiwa kifungo’.

Wanachama hao wametaka kifungo hicho kisomeke ‘Asiwe ametiwa hatiani kwa kifungo cha zaidi ya miezi sita bila mbadala wa adhabu na endapo ametiwa hatiani kwa kifungo cha zaidi ya miezi sita, awe amemaliza muda wa miaka mitano tangu kuisha kwa kifungo husika bila kutiwa hatiani kwa kosa lingine lolote la jinai.

Kipengele hicho (b) kimeongezwa maneno yanayosomeka: ‘Mgombea ni lazima awe ametimiza angalau mwaka mmoja wa uanachama na si miaka mitano kama ilivyo sasa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC