Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MRISHO NGASA FITI KUIVAA AZAM KESHO, KASEJA AAHIDI MAKUBWA GOLINI

MRISHO Ngassa amefanya mazoezi vizuri na kumaliza kuashiria yuko tayari kwa mchezo wa Jumatano dhidi ya Azam FC Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Ngassa aliyewasili kwenye kambi ya timu yake, Yanga SC katika hoteli ya Kiromo, Bagamoyo mkoani Pwani alikosekana katika mchezo uliopita wa ligi hiyo dhidi ya Mtibwa Sugar mjini Morogoro kwa sababu ya majeruhi.

Ngassa alitoka uwanjani kipindi cha pili Jumapili ya wiki iliyopita baada ya kuumia Yanga SC ikimenyana na Al Ahly ya Misri mjini Alexandria katika mchezo wa marudiano Raundi ya Kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika na kutolewa kwa penalti 4-3 kufuatia sare ya jumla ya 1-1.

Na baada ya kutua Dar es Salaam Jumatano, alikwenda Mwanza mapumzikoni, huku wenzake wakiingia kambini kujiandaa na mechi dhidi ya Mtibwa Sugar mjini Morogoro Jumamosi iliyoisha kwa sare ya bila kufungana.

Ngassa anatarajiwa kucheza dhidi ya timu yake ya zamani, Azam FC kwa mara ya kwanza msimu huu baada ya kukosa mechi mbili, ya Ngao ya Jamii Yanga ikishinda bao 1-0 na wa Ligi Kuu mzunguko wa kwanza, Azam FC wakishinda 3-2.


Yanga iliyomleta Ngassa Dar es Salaam kwa mara ya kwanza kutoka Kagera Sugar ya Bukoba mwaka 2007, ilimuuza mchezaji huyo Azam FC mwaka 2009, ambao nao mwaka 2012 wakamtoa kwa mkopo Simba SC kumalizia Mkataba wake.

Baada ya kumalizana na Simba SC,
msimu huu Ngassa amerudi timu yake iliyomuingiza mjini na Jumatano anatarajiwa kukutana na Azam kwa mara ya kwanza tangu arejee Yanga.

Ngassa alikosa mechi za awali dhidi ya Azam FC msimu huu kwa sababu alikuwa anatumikia adhabu ya kufungiwa mechi sita kwa kosa la kuhamia Yanga SC akiwa ana Mkataba na Simba SC.

Mtoto huyo wa kiungo wa zamani wa Pamba FC ya Mwanza na Simba SC, Khalfan Ngassa ‘Babu’ anatarajiwa kuwa kivutio kikubwa kwenye mchezo wa Jumatano iwapo atacheza.

Kipa anayeonekana kuwa chaguo la kwanza Yanga chini ya kocha Mholanzi, Hans van der Pluijm, Deo Munishi ‘Dida’ aliyedaka mechi zote dhidi ya Al Ahly na kupangua penalti mbili Uwanja wa Border Guard, aliumia mkono siku moja kabla ya mechi na Mtibwa na Juma Kaseja akaziba vyema pengo lake.

Wazi sasa Kaseja ndiye atakayepewa jukumu la kuzuia michomo ya Azam Jumatano. Mchezaji mwingine atakayekosekana kwenye mchezo wa keshokutwa ni majeruhi wa muda mrefu, kiungo Salum Telela aliyefunga bao pekee katika mchezo wa Ngao.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC