Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAN UNITED YAZIDI KUMUUMIZA KICHWA MOYES, YAPIGWA 3-0 NA VIJOGOO

KLABU ya Manchester United imeizawadia ushindi wa kwanza Liverpool Uwanja wa Old Trafford baada ya miaka mitano, kufuatia kuchapwa mabao 3-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England.

Kiungo Steven Gerrard amefunga mabao mawili kwa penalti dakika za 34 na 46 wakati Luis Suarez amefunga bao lake la 25 msimu huu dakika ya 84 kukamilisha ushindi mnono wa 3-0.Gerrard alifunga penalti ya kwanza baada ya beki wa United, Rafael kuunawa mpira kwenye eneo la hatari na Nahodha huyo wa Wekundu wa Anfield akafunga tena kwa tuta lingine kufuatia Phil Jones kumchezea rafu Joe Allen kipindi cha pili.

Nahodha huyo wa England angeweza kuifungia Liverpool hat-trick ya kwanza Old Trafford tangu mwaka 1936 kama mkwaju wake wa tatu wa penalti usingegonga mwamba baada ya Nemanja Vidic kumchezea rafu Daniel Sturridge.


Vidic alitolewa nje kwa kadi nyekundu kwa rafu hiyo - hiyo ikiwa mara ya nne anatolewa kwenye mechi dhidi ya Liverpool, ingawa marudio ya picha za Televisheni yalimuonyesha Sturridge akijirusha ili kupata penalti.

Matokeo hayo yanaifanya Liverpool itimize pointi 62 baada ya mechi 29 na kupanda nafasi ya pili, ikiishusha Manchester City yenye pointi 60 za mechi 27 katika nafasi ya nne na Arsenal yenye pointi 62 za mechi 29 sasa ni ya tatu, Chelsea ikiendelea kuongoza kwa pointi zake 66 za mechi 30.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC