Ruka hadi kwenye maudhui makuu

LOGARUSIC AULA SIMBA, AONGEZEWA MWAKA MMOJA ZAIDI

Licha ya timu ya Simba kusuasua kwenye mechi za Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, uongozi wa klabu hiyo ya jijini Dar es Salaam unatarajia kumpa mkataba mpya wa mwaka mmoja kocha mkuu wa timu hiyo, Mcroatia Zdravko Logarusic, imefahamika.

Logarusic aliyetua nchini Desemba mwaka jana, alipewa mkataba wa miezi sita kuifundisha Simba huku akilipwa mshahara wa Dola za Marekani 3,000.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana jijini Dar es Salaam kutoka chanzo chetu kilichopo ndani ya klabu hiyo, zinaeleza kuwa uongozi wa klabu hiyo umeridhishwa na kiwango kilichoonyeshwa na kocha huyo wa zamani wa Gor Mahia ya Kenya.


Chanzo hicho kiliongeza kwamba, uongozi utampa mkataba mpya mara baada ya ligi kumalizika na itampa ruhusa fupi ya kurejea kwao kusalimia familia na kutakiwa kuwahi kurudi nchini kuendelea na zoezi la usajili wa wachezaji.

"Ana nafasi kubwa ya kupewa mkataba mpya, ila itakuwa ni baada ya msimu huu (2013/2014) kumalizika, ingawa kama binadamu ana mapungufu yake," alisema mmoja wa viongozi wajuu wa Simba.

Habari zaidi kutoka Simba zinaeleza kuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa klabu hiyo, Moses Basena, anatarajiwa kuelekea Uganda kwa lengo la  kusaka wachezaji wenye uwezo ili waweze kusajiliwa katika msimu ujao wa ligi.

Katibu Mkuu wa Simba, Ezekiel Kamwaga, aliliambia gazeti hili kuwa ni kweli uongozi umeshaanza kumjadili kocha huyo lakini bado maamuzi rasmi hayajatolewa.

Kamwaga alisema Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo itapitisha maamuzi ya kumpa mkataba mpya Logarusic baada ya kupokea taarifa kutoka kwenye Kamati ya Ufundi.

Alieleza kuwa mkataba wa sasa wa Logarusic unatarajiwa kumalizika Mei 31, mwaka huu.

Logarusic na Kocha Msaidizi, Selemani Matola, walikabidhiwa mikoba ya kuiongoza Simba baada ya Abdallah Kibaden (King) na msaidizi, Jamhuri Kihwelu (Julio) kutimuliwa.

Simba ina pointi 36 na iko katika nafasi ya nne katika msimamo wa ligi hiyo inayoshirikisha timu 14 kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini ambayo itamalizika Aprili 19, mwaka huu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...