Ruka hadi kwenye maudhui makuu

LOGA AITABIRIA UBINGWA YANGA.

Kocha wa Simba, Zdravko Logarusic ‘Loga’ amesema tiketi ya timu yake kufuzu kucheza michuano ya kimataifa ipo mikononi mwa Azam FC, Yanga na Mbeya City.

Awali, Loga ambaye alijiunga na kikosi cha Wekundu hao wa Msimbazi Desemba mwaka jana, aliweka wazi kwamba kikosi chake hakina nafasi ya kutwaa ubingwa msimu huu.

Kwa sasa Simba inakamata nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi Kuu ikiwa na pointi 36, baada ya kucheza mechi 21, kati ya hizo kushinda tisa, kutoka sare tisa na kupigwa mara tatu,  kama Simba watashinda mechi zake zote tano itafikisha pointi 51.

Azam FC inakamata uongozi wa ligi hiyo ikiwa na pointi 40 wakiwa na mechi nne mkono, Mbeya City ni ya pili ikiwa na pointi 39 na Yanga ni ya tatu ikiwa na pointi 38.

Hata hivyo, Yanga inapewa nafasi zaidi ya kunyakua taji hilo kutoka kutokana na kusaliwa na michezo mitano  mkononi.


Loga alisema: “Sina uhakika kama tutashiriki mashindano ya kimataifa au la kwa sababu tulifanya makosa makubwa kupoteza mechi mbili.

“Ok, tuna uwezo wa kushinda mechi zote zilizosalia, lakini hiyo pekee haiwezi kutupa nafasi ya kushiriki mashindano ya kimataifa isipokuwa pale tu wenzetu walioko juu yetu watakapovurunda,” alisema Loga

Aliongeza: “Tutakachofanya sisi ni kupambana hadi mwisho baada ya hapo  tutajua nafasi yetu,” alisema Loga ambaye anasemekana ataikacha Simba mwisho wa msimu wakati mkataba wake wa miezi sita utakapofikia ukingoni.

Katika hatua nyingine, Loga alisema ataendelea kusimamia misingi ya taaluma yake licha ya kwamba anafahamu wapo wasiofurahishwa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC