Ruka hadi kwenye maudhui makuu

JINAMIZI LA WAARABU LAZIDI KUITESA YANGA.

BAO la dakika ya 83 la kinda Kevin Friday limeinusuru Azam FC kulala mbele ya Yanga SC baada ya kulazimisha sare ya kufungana 1-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Azam ilicheza kwa zaidi ya dakika 20 za mwisho ikiwa pungufu baada ya beki wake wa kulia, Erasto Nyoni kutolewa nje kwa kadi nyekundu kwa kutoa lugha chafu kwa refa.

Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa askari wa jeshi la Polisi Tanzania, Hashim Abdallah wa Dar es Salaam aliyesaidiwa na Anold Bugado wa Singida na Florentina Zablon wa Dodoma, hadi mapumziko tayari Yanga walikuwa mbele kwa bao 1-0.

Bao hilo lilifungwa na mshambuliaji kutoka Burundi, Didier Kavumbangu dakika ya 14 aliyekutana na mpira uliorudi baada ya kupanguliwa na kipa Aishi Salum Manula kufuatia kutokea piga nikupige langoni mwa Azam.


Shambulizi lililozaa bao hilo lilianzia kwa kwa Simon Msuva aliyemtoka beki Gadiel Michael wingi ya kulia na kutia krosi iliyounganishwa na Kavumbangu lakini mpira ukagonga mwamba na kurudi uwanjani na kumkuta Hamisi Kiiza aliyepiga kipa akaokoa na kumkuta mfungaji aliyemaliza kazi.

Azam FC ilikosa mabao mawili ya wazi kipindi cha kwanza, wakati bao lililofungwa na Kipre Herman Tchetche refa Hashim alikataa kwa sababu mpigaji kabla ya kufumua shuti alimsukuma beki Kevin Yondan.

Wachezaji wa Azam mara mbili walimfuata refa Hashim kumlalamikia kwa kutoridhishwa na uamuzi wake, mfano alipokataa bao na mara moja alipokataa kutoa mpira wa adhabu baada ya John Bocco kuangushwa karibu na eneo la hatari.

Kipindi cha pili timu zote ziliingia na vikosi vile vile, Azam wakiendelea kusaka bao la kusawazisha na Yanga wakitaka kunenepesha ushindi wao.

Hata hivyo, nyota ya Yanga SC iliendelea kung’ara baada ya kupata penalti dakika ya 69 kufuatia beki Said Mourad ‘Mweda’ kuunawa mpira uliopigwa na Didier Kavumbangu, hata hivyo mkwaju wa Hamisi Kiiza ‘Diego’ ulipanguliwa vizuri na kipa Aishi Salum Manula na kuwa kona ambayo haikuzaa matunda.

Baada ya kona hiyo wachezaji wa Azam wa Azam FC walikwenda kumlalamikia refa ambaye alimuonyesha kadi ya pili ya njano Erasto Nyoni na kuwa nyekundu.

Pamoja na kubaki wachache, Azam waliendelea na jitihada za kusaka bao la kusawazisha na dakika ya 83 kinda aliyepandishwa kutoka kikosi cha pili, Kevin Friday aliipokea vyema pasi ya Salum Abubakr ‘Sure Boy’ na kumchambua kipa mkongwe Juma Kaseja.

Kutoka hapo Azam walicharuka zaidi na kufanya mashambulizi mawili zaidi, lakini hawakufanikiwa kupata bao.

Kwa ujumla mchezo ulikuwa mkali na wa ushindani- wenye hadhi ya Ligi Kuu kweli. Azam FC sasa inajiongezea pointi moja na kufikisha pointi 44 baada ya mechi 20, wakati Yanga SC inatimiza pointi 40 baada ya mechi 19.
 
Kikosi cha Yanga SC kilikuwa; Juma Kaseja, Juma Abdul, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Frank Domayo, Simon Msuva, Hassan Dilunga, Didier Kavumbangu/Mrisho Ngassa dk73, Hamisi Kiiza/Hussein Javu dk87 na Emmanuel Okwi.

Azam FC; Aishi Manula, Erasto Nyoni, Gadiel Michael, Said Mourad, Kipre Balou, Himid Mao, Salum Abubakar, John Bocco, Kipre Tchetche na Khamis Mcha/Kevin Friday dk49.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...