Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AZAM YAZIDI KUPAA KILELENI

AZAM FC imepiga hatua kuikimbia Yanga SC katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kufuatia kuifunga JKT Oljoro bao 1-0 jana Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Matokeo hayo yanaifanya Azam FC itimize pointi 47 baada ya kucheza mechi 21, ikiwazidi mabingwa watetezi, Yanga SC kwa pointi nne ambao hata hivyo wana mechi moja mkononi.

Shujaa wa Azam FC hiyo jana alikuwa ni John Bocco ‘Adebayor’ aliyefunga bao hilo peke dakika ya 71 kwa shuti kali baada ya kupokea pasi ya kinda Kevin Friday.

Azam FC ilipoteza nafasi nyingi za wazi kupitia kwa Brian Umony dakika ya tisa, Khamis Mcha ‘Vialli’ dakika ya 11, Kipre Tchetche dakika ya 13, John Bocco ‘Adebayor’ dakika ya 39.


JKT Oljoro ilifika kwenye lango la Azam mara moja tu dakika ya 33, baada ya pasi ya Iddi Swalehe kumfikia Shijja Mkina, lakini shuti lake likadakwa na kipa Aishi Salum Manula.
 
Kipindi cha pili, kocha Mcameroon wa Azam FC, Joseph Marius Omog alianza na mabadiliko, akimpumzisha mshambuliahji Mganda, Brian Umony dakika ya 49 ambaye bafasi yake ilichukuliwa na kinda Kevin Friday.

Omog aliwapumzisha pia Khamis Mcha ‘Vialli’ dakika ya 58 na nafasi yake kuingia Mudathir Yahya, wakati Brison Raphael alimpisha Gaudence Mwaikimba dakika ya 73.
 
Kikosi cha Azam FC; Aishi Manula, Himid Mao, Gadiel Michael, Said Mourad, David Mwantika, Brison Raphael/Gaudence Mwaikimba dk73, Khamis Mcha ‘Vialli’/Mudathir Yahya dk58, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, Brian Umony/Kevin Friday dk49, John Bocco ‘Adebayor’ na Kipre Tchetche.

JKT Oljoro; Mohamed Ally, Naplo Zuberi, Ally Hamza, Nurdin Suleiman, Shaibu Nayopa, Jacob Raymond, Hamisi Maulid/Babu Ally dk68, Amir Omary, Shija Mkinna/Juma Mohammed dk62, Yussuf Machogore na Iddi Swalehe.

Katika mechi nyingine, Simba SC imefungwa 1-0 na Coastal Union Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam bao pekee la Hamad Juma dakika ya 44, Ruvu Shooting imeifunga 2-0 Ashanti United Uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Pwani mabao ya Elias Maguri dakika za sita na 63 wakati Mgambo JKT imetoka sare ya 1-1 na Mtibwa Sugar ya Morogoro Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...