Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TUTAIUA AL AHLY KAMA KOMOROZINE- OKWI

Na Fikiri Salum

Kama walivyotoa ahadi ya mabao kwenye mchezo wa ligi kuu bara kati yao na Ruvu Shooting ambapo wachezaji wa Yanga waliahidi kuifunga magoli mengi timu hiyo, ndivyo itakavyokuwa katika mchezo wa klabu bingwa barani Afrika kati ya mabingwa wa Tanzania bara na wawakilishi pekee katika michuano ya kimataifa Yanga dhidi ya mabingwa watetezi wa Afrika Al Ahly ya Misri.

Yanga na Al Ahly ya Misri zitakutana kesho kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ambapo wachezaji wa mabingwa hao wa bara wameahidi kuishushia kichapo kitakatifu Al Ahly kama waliofanyia Komorozine ya Comoro.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Emmanuel Okwi raia wa Uganda amesema ana usongo mkubwa katika michuano ya kimataifa na hasa mechi iliyo mbele yake, Okwi ametamba kutoka na magoli si zaidi ya mawili katika mechi hiyo kwani wapinzani wao ni timu ya kawaida kama nyingine, Naye Simon Msuva amedai Al Ahly ni timu ya kawaida na inafungika.



'Katika mchezo huo lengo langu ni kupeleka mashambulizi mengi langoni mwao na ikiwezekana na mimi nifunge moja au mawili, nawaambia mashabiki wa Yanga waje washuhudie kalamu ya magoli uwanja wa Taifa', alisema Msuva ambaye amekuwa katika kiwango cha juu siku za hivi karibuni.

Mrisho Ngasa ambaye anaongoza kwa magoli barani Afrika ametamba kutoka na goli zake mbili ama tatu katika mchezo huo huku akiahidi mvua ya magoli kuendelea, 'Tutashinda tu katika mechi hiyo, Yanga hii si timu ya kuichezea ni moto wa kuotea mbali tena tutafunga mengi, ni msimu wetu kusonga mbele', alisisitiza Ngasa.

Kocha msaidizi wa Yanga Charles Boniface Mkwasa amesema Al Ahly ni timu ya kawaida sana na ameiona ilipocheza na Sfaxien katika fainali ya Super Cup, 'Ni timu ya kawaida na inawezekana tukaifunga, kuhusu goli ngapi hiyo ni mipango ya mungu lakini lazima tuwafunge, nimezijua mbinu zao na tutazifanyia kazi', aliongeza Mkwasa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC