Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TFF KUMRUHUSU OKWI KUKIPIGA YANGA.

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limesema linajipanga kulipigia simu Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) kusaka ufafanuzi wa uhalali wa usajili wa mshambuliaji Emmanuel Okwi kwa klabu ya Yanga.

Januari 22 mwaka huu ikiwa ni siku mbili tu kabla ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF ilisimamisha usajili wa Mganda huyo katika klabu ya Yanga wakati likisubiri ufafanuzi Fifa.

Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura amesema jana mchana jijini hapa kuwa baada ya kusubiri kwa muda mrefu pasipo kupewa ufafanuzi wowote, wameamua kulitwangia simu shirikisho hilo la kimataifa.


"Suala la Okwi bado halijapata ufumbuzi kwa sababu hatujajibiwa chochote na Fifa mpaka sasa, kwa kuwa tumeshaandikia barua kuwakumbusha tunahitaji ufafanuzi na hawajatujibu, itabidi tuwapigie simu," amesema Wambura.

"Fifa ni taasisi kubwa, pengine wanahitaji kukumbushwa kuhusu suala hilo ndiyo maana tumeamua tuwapigie simu ili tujue limefikia wapi na ikiwezekana watu au kamati inayolishughulikia," amesema zaidi Wambura bila kueleza siku ambayo shirikisho hilo litapiga simu Fifa.

Okwi, ambaye aliingia mgogoro na klabu yake ya Etoile du Sahel (ESS) ya Tunisia aliruhusiwa na Fifa kuchezea SC Villa kwa kibali maalumu (provisional permit) cha miezi sita ili kulinda kiwango chake wakati suala lake dhidi ya klabu hiyo ya Tunisia likishughulikiwa na shirikisho hilo la kimataifa.

Lakini, SC Villa ilimuuza mchezaji huyo wa zamani wa Simba kwa mkataba wa miaka miwili na nusu kwa Yanga Desemba mwaka jana akiwa ametumikia miezi minne kati ya sita aliyoruhusiwa na Fifa kukaa katika klabu hiyo ya Uganda.

Wakati hali hiyo ikiendelea katia ya Yanga na TFF, klabu ya Simba nayo haijalipwa dola za Marekani 300,000 (Sh. milioni 480) za mauzo ya mshambuliaji huyo hatari kwa kufumania nyavu kwa ESS tangu Januari mwaka jana ilipowauzia wawakilishi hao wa Tunisia katika mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC