Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ROONEY KUONGEZA MKATABA MAN UNITED

Wayne Rooney 

Wayne Rooney anatarajiwa kutia saini mkataba mpya wiki hii ambao utaweka straika huyo wa Uingereza katika Manchester United hadi mwisho wa msimu wa 2018-2019, vyombo vya habari nchini humo viliripoti Jumatatu.

Mchezaji huyo wa miaka 28 huenda atie saini mkataba huo Old Trafford Jumatano au Alhamisi, Chama cha Wanahabari kilisema.

Kumekuwepo na shaka kuhusu mustakabali wa Rooney katika miamba hao wa Ligi Kuu ya Uingereza hasa baada ya Chelsea kujaribu kumshawishi ajiunge nao kabla ya kuanza kwa msimu huu.

Licha ya masaibu ya United kwa sasa mbele ya meneja mpya David Moyes – ambayo yamepelekea wao kukwama nambari saba, alama 15 nyuma ya viongozi Chelsea – Rooney anadaiwa kutulia Old Trafford.


Mapema mwezi huu, Rooney alisisitiza kwamba “anaangazia uchezaji soka” huku uvumi ukitanda kuhusu mashauriano kuhusu mkataba wake, ambao unafikia kikomo mwisho wa msimu ujao.
Hata hivyo, alikiri kwamba ana azma ya kuvunja rekodi ya Bobby Charlton ya ufungaji mabao katika klabu. Charlton alifungia United mabao 249 na Rooney kwa sasa ana 208.

"Ni lengo kuu sana kwangu kujaribu kutimiza na kuvunja rekodi ya Sir Bobby, katika klabu na kimataifa,” alisema Rooney, ambaye amepungukiwa na magoli 11 pekee kuvunja rekodi ya Charlton aliyofungia Uingereza ambayo ni 49.”
"Ni jambo ambalo ningependa sana kufanya. Kama naweza kufanya hilo, ninaweza kujionea fahari sana, kwa sababu imedumu kwa muda mrefu.”

Rooney alianza uchezaji wake wa kulipwa akiwa na umri wa miaka 16 akiwa Everton chini ya Moyes na ametetea meneja huyo anayekabiliwa na shinikizo msimu wake wa kwanza, baada yake kushindwa kuendeleza ufanisi wa Alex Ferguson.

"David Moyes ni meneja mzuri ajabu," Rooney alisema wiki iliyopita.
"Nilifanya kazi naye nikiwa Everton na kwa miezi kadha hapa United. Amefanya kila awezalo, lakini wachezaji wake ndio wanaofaa kufanya zaidi na natumai kwamba tunaweza kufanya hilo.”

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC