Ruka hadi kwenye maudhui makuu

PISTORIUS AJUTIA KIFO CHA MPENZI WAKE

Oscar Pistorius
DUNIA leo inaadhimisha siku ya wapendanao yaani Valentine Day, Mwanariadha wa Afrika Kusini Oscar Pistorius, amezungumzia masikitiko na majuto yake kuhusu mauaji ya aliyekuwa mpenzi wake Reeva Steenkamp, mwaka mmoja uliopita.

Katika taarifa kwa mtandao wake, alisema: ''Kumpoteza Reeva kulinipa huzuni mkubwa sana siku hiyo na nitaubeba maisha yangu yote.''

Kesi ya mauaji dhidi ya Pistorius inatarajiwa kuanza mjini Pretoria mnamo mwezi Machi.
Oscar anasema kuwa alimpiga risasi Reeva kwa bahati mbaya baada ya kudhani kuwa alikuwa jambazi ndani ya nyumba yake alipompiga risasi kupitia mlango wa bafu yake mwaka 2013.
Mwendesha mkuu wa mashitaka anadai kuwa mauaji hayo yalikuwa ya kupangwa baada ya wawili hao kuzozana.


Huenda akafungwa jela maisha ikiwa atapatikana na hatia.

Nini kilitendeka usiku huo?

Kukamatwa kwa Pistorius mwaka jana kuliwashangaza wengi sana nchini Afrika Kusini na duniani kote hasa kwa wale waliomuona kama mwanamichezo mahiri na ambaye ni kioo cha jamii hasa baada ya kuteta kwa miaka mingi na kutaka aruhusiwe kushiriki michezo.

Mwanamichezo huyo mwenye umri wa miaka 27, alishinda medali ya dhahabu katika michezo ya Olimpiki ya walevamu mwaka 2012 na pia kwenye michezo ya Olimpiki.
Mepama wiki hii, familia ya Reeva ilisema kuwa mamake June atahudhuria kesi dhidi ya Pistorius ambayo inatarajiwa kuanza tarehe 3 mwezi Machi.

Reeva Steenkamp, alikuwa mwanamitindo mwenye umri wa miaka 29. Alipigwa risasi mara tatu alipokuwa bafuni nyumbani mwa Pistorius tarehe 14 Februari 2013.

Pistorius alisema kuwa alidhani mtu aliyeingia nyumbani kwake alikuwa jambazi na anakana madai kuwa walikosana na Reeva masaa za asubuhi siku hiyo kabla ya kumpiga risasi.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC