Ruka hadi kwenye maudhui makuu

OKWI KUONGOZA MAUAJI YANGA LEO

Yanga leo inashuka kwenye Uwanja wa Taifa kucheza na Ruvu Shooting huku kocha mkuu wa timu hiyo, Hans Van der Pluijm akipanga kumtumia mshambuliaji Emmanuel Okwi kwa mara ya kwanza kwenye michezo ya ligi kuu ya Bara.

Okwi hajaichezea timu hiyo mchezo wowote wa ligi tangu alipotua timu hiyo katika dirisha dogo la Januari kutokana na utata uliokuwapo kwenye usajili wake.

Afisa Habari wa klabu hiyo, Baraka Kizuguto, alisema Pluijm anaweza akamtumia Okwi leo kulingana na mahitaji yake.

"Suala la Okwi kucheza au kutocheza hilo lipo mikononi mwa kocha kulingana na kikosi chake atakachokipanga kesho," alisema Kizuguto kwa sababu "kocha kwa sasa yupo huru kumtumia na kutokana na mazoezi ya leo (jana) asubuhi ni wazi atamtumia."


Aidha, Kizuguto alisema Pluijm anajivunia ushirikiano na umoja wa wachezaji wake wanaoendelea kuuonyesha klabuni hapo.

Mashabiki wa klabu hiyo wana hamu kubwa ya kumuona kwenye ligi mshambuliaji Mganda huyo ambaye alifanya vizuri akiwa na klabu yake ya zamani ya Simba hapa nchini kabla ya kuuzwa kwa klabu ya Etoel du Sahel ya Tunisia miezi 13 iliyopita.

Yanga inavaana na Ruvu Shooting ikitokea kwenye mashindano ya kimataifa ambapo iliitoa Komorozine ya Comoro kwa jumla ya magoli 12-2 kwenye raundi ya awali ya Ligi ya Klabu Bingwa Afrika.

Van Pluijm alisema michezo ya ligi kuu ni sehemu ya maandalizi kabla ya kuvaana na mabingwa watetezi Al-Ahly ya Misri Jumamosi ijayo katika mechi ya raundi ya kwanza ya michuano hiyo ya Afrika.

Mbali na kutumia ligi kuu ya Bara kama mazoezi ya maandalizi, timu hiyo ilimtuma kocha msaidizi Charles Mkwasa Misri kushuhudia mchezo wa Super Cup kati ya Alhy na mabingwa wa Kombe la Shirikisho la klabu za Afrika CS Sfaxien ya Tunisia.

Mkwasa aliyerejea jana, alitumwa kuwasoma mabingwa mara nane hao Afrika kabla ya kuvaana nao Machi mosi.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC