Ruka hadi kwenye maudhui makuu

OKWI, KIIZA WAULA UGANDA, OWINO WA SIMBA ATOSWA

KOCHA Mserbia, Milutin Sredojevic ‘Micho’ amewaita wote washambuliaji wa Uganda waliopo kwenye kikosi cha Yanga SC ya Dar es Salaam, Emmanuel Arnold Okwi Hamisi Friday Kiiza ‘Diego’ kwa ajili ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Zambia, Chipolopolo ulio katika kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) utakaofanyika Machi 5, mwaka huu Uwanja wa Ndola, Zambia.

Katika taarifa aliyotumwa mapema jana, Micho amewachunia beki wa Simba SC, Joseph Owino na washambuliaji Brian Umony wa Azam FC na Yayo Lutimba wa Coastal Union, Waganda wengine wanaocheza Tanzania.

Kikosi kamili kwa ajili ya mechi hiyo alichoteua Micho ni makipa; Onyango Dennis wa Bidvest Wits ya Afrika Kusini, Odonkara Robert wa Saint George ya Ethiopia na Watenga Ismail wa Vipers.

Mbakei ni Iguma Denis wa Victoria University, Wadada Nicholas wa Vipers, Walusimbi Godfrey wa Gor Mahia ya Kenya, Kakuba Alex wa Covilha ya Ureno, Kalungi Henry wa Richmond Kickers ya Marekani, Isinde Isaac wa Saint George, Mwesigwa Andrew wa Ordabasy ya Kazakhstan, Kassaga Richard wa Kira Young na Ochaya Joseph wa Asante Kotoko ya Ghana.


Viungo ni Mawejje Tony wa Haugesund ya Norway, Aucho Khalid wa Tusker, Kizito Geoffrey wa Gor Mahia za Kenya na Ntege Ivan wa KCC, wakati viungo wa pembeni na washambuliaji ni Oloya Moses, Kizito Luwagga William wa Covilha ya Ureno, Matovu Sula wa BK Hacken ya Sweden, Majwega Brian wa KCC, Massa Geoffrey wa University of Pretoria ya Afrika Kusini, Okwi, Kiiza, Sserunkuma Dan wa Gor Mahia na Odour Tony wa KCC.

Ikumbukwe Yanga SC itacheza mechi ya marudiano na Al Ahly ya Misri mjini Cairo kati ya Machi 7 na 9 katika Raundi ya Kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya mchezo wa kwanza Dar es Salaam Machi 1, mwaka huu.

Kwa Micho kuwaita Kiiza na Okwi dhahiri itaathiri maandalizi ya Yanga kwa ajili ya mchezo wa marudiano na Ahly, kwani watalazimika kwenda Uganda mara tu baada ya mechi ya kwanza na mabingwa hao wa Afrika na kwa kuwa watacheza mechi Ndola Machi 5, maana yake wanaweza kuondoka huko Machi 6 wakati tayari mabingwa wa Bara wakiwa Cairo.

Okwi na Kiiza hawatapata fursa ya kushiriki mazoezi ya Yanga kujiandaa na mchezo wa marudiano na Ahly, pia watachoka na safari na mechi ngumu mfululizo.

Tanzania pia itakuwa na mechi katika tarehe ya FIFA na kama kocha Mdenmark Kim Poulsen ataita wachezaji wa Yanga kwa utaratibu wake wa kambi ya wiki nzima kabla ya mechi, ina maana kambi ya maandalizi ya klabu hiyo itapata pigo kubwa, kwa kuwa kwa sasa wachezaji wengi wa Stars hutokea timu hiyo ya Jangwani.

Hali itakuwa mbaya zaidi kwa Yanga iwapo na Rwanda itawaita Mbuyu Twite na Haruna Niyonzima kwa ajili ya mechi za wiki ijayo za kalenda ya FIFA.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC