Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NGASA AMFUNIKA OKWI YANGA.

BAADA ya mechi 20 za kuichezea klabu ya Yanga SC ya Dar es Salaam tangu arejee msimu huu, Mrisho Khalfan Ngassa amedhihirisha klabu hiyo haikukosea kumrejesha Jangwani.

Jumapili Ngassa alicheza mechi ya 20 tangu arejee Yanga SC msimu huu akitokea kwa mahasimu, Simba SC alikocheza msimu mmoja akitokea Azam FC, waliomtoa Jangwani mwaka 2009.

Ngassa alifunga mabao matatu katika ushindi wa 5-2 mjini Moroni, Comoro dhidi ya wenyeji, Komorozine katika mchezo wa marudiano Raundi ya Awali, Ligi ya Mabingwa Afrika.

Katika mechi hizo 20, Ngassa ametimiza mabao 15 na kuwapiku wachezaji kadhaa waliomtangulia, huku kukiwa kuna kila dalili atampiku Mrundi Didier Kavumbangu, mchezaji mwenye mabao mengi kati ya nyota waliojiunga na timu hiyo ndani ya misimu hii miwili.


WANAOONGOZA KWA MABAO YANGA

D. Kavumbangu Yanga   25 52
Mrisho Ngassa Yanga 15 20
Said Bahanuzi Yanga 14 39 
Simon Msuva Yanga 10 50
Nizar Khalfan Yanga 7 31
Emmanuel Okwi Yanga 3 4
Mbuyu Twite Yanga 3 52
Hussein Javu Yanga 2 9
(Orodha hii inawahusu wachezaji waliosajiliwa Yanga SC ndani ya misimu hii miwili tu)


Kavumbangu ameifungia Yanga mabao 25 katika mechi 52 za kirafiki na mashindano yote alizoichezea timu hiyo tangu ajiunge nayo msimu uliopita, moja likiwa la penalti.

Ngassa ambaye msimu uliopita akiwa Simba SC alifunga mabao saba ndani ya mechi 27, tayari amempiku Said Bahanuzi ambaye ameifungia Yanga mabao 14 katika mechi 39 ndani ya misimu miwili, yakiwemo matatu ya penalti.

Simon Msuva anashika nafasi ya nne kwa mabao yake 10 ndani ya mechi 50, Nizar Khalfan wa tano kwa mabao yake saba ndani ya mechi 31, nyingi akitokea benchi, Emmanuel Okwi wa sita kwa mabao yake matatu ndani ya mechi nne sawa na Mbuyu Twite aliyecheza mechi 52 wakati Hussein Javu amefunga mabao mawili ndani ya mechi tisa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC