Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MMAREKANI ANYAKUA TUZO YA FIFA 2014 WORLD CUP SUPER SONG COMPETETION.

Na Regina Mkonde

Msanii kutoka marekani anayefahamika kwa jina la Elijah King, juzi aliibuka mshindi kwa kunyakua tuzo ya Super Song iliyoandaliwa na shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA.

Nyimbo iliyompa ushindi mwanamuziki huyo ni nyimbo ya VIDA, Nyimbo ambayo mashairi yake yamesimama na ya kuvutia kiasi kwamba ikazifunika nyimbo nyingine zote zilizokuwa zinashindania tuzo hiyo.

Kutokana na ubora wa nyimbo hiyo iliwaweka majaji hao katika wakati mgumu kuchuja na nyimbo nyingine, Na kuzidi kuipa nafasi nyimbo hiyo kwa kura nyingi hatimaye juzi kuibuka mshndi wa nyimbo bora ya FIFA 2014 WORLD CUP SUPER SONG COMPETETION.

Mashindano hayo ambayo juzi yalikuwa fainali ambapo staa Ricky Martin, alipomtangaza rasmi Mmarekani huyo kuwa ni mwanamuziki bora wa FIFA mwaka 2014.Na wimbo wake kuwa ni wimbo bora katika mashindano hayo.


Kutokana na tuzo hiyo FIFA imempa shavu mwanamuziki huyo ya kufanya kazi na maprodyuza machachari wa Super Song, ambao ndio hao waliouandaa wimbo huo bora wa FIFA.pamoja na kufanya kazi na Global Super star anayefahamika kwa jina la Ricky Martin.

Elijah King pia amepata shavu la kuwa mgeni rasmi(V.I.P) na kupata ofa ya tiketi ya kuhudhuria bure michuano ya fainali ya kombe la dunia itakayo fanyika nchini Brazil itakayo anza mwanzoni mwa mwezi wa sita mwaka huu.

Elijah King alifurahi sana na kuishukuru FIFA juu ya mashindano hyo waliyoyaandaa, maana imeleta changamoto kubwa katika maendeleo ya kazi zake na kumfanya azidi kuwa kinara na kutambulika dunia nzima.

Si jambo la kushangaza mmarekani huyo kupata tuzo hiyo,hususani katika ulimwengu huu wa sasa  wamarekani ndiyo wanaoongoza na kuwa kinara katika tasnia ya muziki.

Elijah King kupata tuzo hiyo ni changamoto kubwa aliyoipata kutokana na mashindano yalikuwa na ushindani wa hali ya juu,kutokana na asilimia kubwa ya magwiji wa muziki duniani kuwania tuzo ya mashindano hayo.

Wanamuziki wakubwa kama Rihana n.k nao pia walikuwa wanaigombea tuzo hiyo, lakini mwisho wa siku staa huyo kuibuka kidedea. Na kuwaacha nyota hao na mshangao. 

Hivyo basi michuano hiyo ikianza tutazidi kuusikia wimbo huo bora unafahamika kwa jina la vida.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC