Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MBEYA CITY WAPIGA KAMBI MOMBASA KUIUA COASTAL UNION KESHO

Na Salum Fikiri Jr

Kikosi cha Mbeya City kimeweka kambini jijini Mombasa, Kenya kwa ajili ya mechi yao ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Coastal Union itakayochezwa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga kesho.

Msemaji wa Mbeya City, Fred Jackson alisema jana kuwa, kikosi chao kinachonolewa na kocha mzawa, Juma Mwambusi kitakuwa kikijifua jijini Mombasa hadi kesho asubuhi kitakaposafiri kwa basi kwenda jijini Tanga kuwakabili Coastal Union jioni.

"Tulianza safari yetu kuelekea Kenya jana (juzi), tumelala Dar es Salaam. Asubuhi hii tunaunganisha ndege kwenda Mombasa ambako timu itakaa hadi Jumamosi asubuhi," alisema Jackson.


Alisema lengo la kambi hiyo ni kuwafanya wachezaji wao wazoee hali ya hewa ya Mombasa ambayo inawiana na Tanga ambako watawakabili mabingwa wa Tanzania Bara 1988, Coastal Union wanaonolewa na kocha Mganda Yusuph Chipo baada ya kuachana na Hemed Morocco mzunguko wa kwanza.

Wababe hao wa ligi kuu kutoka jijini Mbeya wanakamata nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi hiyo wakiwa na pointi 35 sawa na mabingwa watetezi Yanga walioko nafasi ya pili.

Coastal iliyokuwa imeweka kambi mjini Muscat, Oman kwa ajili ya mzunguko wa pili wa ligi iko nafasi ya saba ikiwa ni baada ya kukusanya pointi 22 katika mechi 18.

Waliokuwa wawakilishi wa Tanzania Bara katika mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika, Azam FC wanakamata usukani wakiwa na pointi 36 baada ya kucheza mechi 16 sawa na Yanga.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC