MAN CITY YAFUNGWA NYUMBANI NA BARCELONA

Kipa Joe Hart na mshambulizi wa Barcelona Messi
Matumani ya timu ya Manchester City kunyakuwa taji la ligi ya mabingwa ulaya yalipata pigo baada ya wachezaji wa Barcelona Lionel Messi na Dani Alves kufunga jumla ya mabao mawili katika mechi iliyochezwa katika uwanja wa Etihad.

Messi alikuwa wa kwanza kufunga kupitia penalty katika dakika ya 54 alipoangushwa na difenda Martin Demichelis aliyepewa kadhio nyekundu.
Licha ya Manchester City kuwa kasoro mchezaji mmoja walijizatiti kukabiliana na timu hiyo ya Uhispania ila Dani Alves alizima matumaini yao mbele ya mashabiki wao alipofunga bao la pili mwisho mwisho wa kipindi cha pili.


Ili kuingia robo fainali itahithitajika kuichapa Bercalona mabao matatu kwa bila.
Katika mechi nyingine ya timu hizo kumi na sita, nchini Ujerumani Bayer Liverkusen iliicharazwa mabao mane kwa bila na Paris Saint Germain ya Ufaransa. Mabao matatu yalifungwa kipindi cha kwanza na la nne katika kipindi cha pili.

Leo Arsenal ambao wako katika nafasi ya pili kwenye ligii ya Uingereza itacheza dhidi ya bingwa mtetezi wa kombe hilo Beyern Munich wakati AC Millan ya Italia itakuwa ikipambana Atletico Madrid ya Uhispania.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

STAA WETU: JEREMIA JUMA MTOTO WA JUMA MGUNDA ALIYEIKACHA SIMBA NA KUENDELEA NA UASKARI